VAN PERSIE AIPAISHA MAN UNITED
Robin van Persie |
Vinara wa ligi kuu England Manchester United wameendeleza wimbi la ushindi baada ya
kuwachapa mahasimu wao Liverpool kwa magoli 2 – 1 katika mechi ya ligi kuu
England.
Man United
ambao walikuwa nyumbani Old Trafford walipata goli lao la kwanza dakika ya 19
kupitia kwa Robin van Persie aliyepata pasi kutoka kwa Patrice Evra, bao ambalo
lilidumu hadi mapumziko.
Dakika ya 54 beki Nemanja Vidic aliifungia goli la
pili Man U baada ya pasi ya mwisho kutoka kwa Patrice Evra, Hata hivyo shangwe
za goli hilo kwa mashabiki wa Red Devils hazikudumu kwani Dani Sturridge
aliifungia Liverpool goli la kufutia machozi dakika ya 57.
Kwa matokeo hayo Man United imefikisha pointi 55
kileleni huku Liverpool ikibakia na pointi zake
ARSENAL YAANGUKIA PUA NYUMBANI
Adin Dzeko |
Katika mechi nyingine ya "Super Weekend" nchini
England ilikuwa baina ya washika bunduki wa London Arsenal dhidi ya Manchester
City ambapo wenyeji Arsenal wamekubali kichapo cha magoli 2 – 0 mechi ikichezwa
katika dimba la Emirates.
Arsenal ilipata pigo mapema kabisa dakika ya tisa
pale beki wake alipolimwa kadi nyekundu kwa kumfanyia madhambi ndani ya penati
boksi Edin Dzeko ambapo Mwamuzi aliamuru penati kupigwa. Edin Dzeko alipiga penati hiyo ambayo iligonga mwamba
na kuokolewa na golikipa wa Arsenal.
James Milner Miner akaifungia goli la kwanza Man City
huku Edin Dzeko akirekebisha makosa kwa
kuifungia goli la ushindi.
Baada ya kucheza kwa kipindi kirefu ikiwa pungufu
dakika ya 74 mzimu wa kadi nyekundu ukawaangukia Man City ambapo nahodha na beki wake Vincent
Kompany alioneshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mbaya Jack Wilshere.
Kwa matokeo hayo Man City imefikisha pointi 48
ikiendelea kujikita katika nafasi ya pili.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil NENE anataraji kujiunga na klabu ya
Al Gharafa ya Qatar akitokea Paris St Germain ya Ufaransa.
NENE(31) aliifungia PSG magoli 21 msimu uliopita, anataraji kusaini
mkataba wa miezi 18 ambao utampatia kiasi cha Euro milioni 16.
Mchezaji huyo ameichezea PSG mechi 79 na kuifungia magoli 36 lakini msimu
huu amecheza mechi tisa tu.
Matokeo
mengine ya ligi kuu England.
|
Queens Park Rangers
|
0-0
|
Tottenham
|
||||||
|
Aston Villa
|
0-1
|
Southampton
|
||||||
|
Everton
|
0-0
|
Swansea
|
||||||
|
Reading
|
3-2
|
West Bromwich Albion
|
||||||
|
Norwich
|
0-0
|
Newcastle United
|
||||||
|
Stoke
|
0-4
|
Chelsea
|
||||||
|
Fulham
|
1-1
|
Wigan
|
0 comments:
Post a Comment