THOMAS MASHALI ATETEA UBINGWA WA AFRIKA MASHARIKI.
Bondia Mtanzania Thomas Mashali ameweza kuutetea mkanda wake wa ubingwa wa Afrika Mashariki na kati baada ya kumtwanga Mkenya Benard Mackoliech katika pambano kali na la kusisimua lililopigwa katika ukumbi wa Friends Corner Manzese jumamosi usiku.
Pambano lilikuwa kali lakini  kukosekana umakini (timing mbovu)  kwa  Benard zilimfanya alambe sakafu karibu mara tatu katika raundi ya nne,tano na sita ambapo alisalimu amri baada ya kuhesabiwa na Mwamuzi Mark Hatia.


Bondia Mtanzania Thomas Mashali kushoto akiwa amemlambisha sakafu  Mkenya  Bernad Mackoliech na kwenda chini akimsubiri ainuke wakati wa mchezo wao wa kugombania ubingwa wa Afrika Mashariki uliofanyika katika ukumbi wa Friends Conner, Manzese jijini Dar es Salaam na Mashali kuibuka na ushindi kwa KNOCK OUT katika raundi ya sita.

Kama vile sako la nyani ngedere haponi hapa mabondia Bernad Mackoliech wa kenya na Mtanzania Thomas Mashali wakioneshana ufundi wa kutupiana makonde wakati wa mchezo wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki Mashali alishinda kwa K,O raundi ya sita.

 Hapa mwamuzi anaonekana akimhesabia tena bondia Bernad toka Kenya baada ya kulambishwa sakafu kwa mara nyingine hii ilikuwa raundi ya sita na akasalimu amri na kumpa ushindi Thomas Mashali wa Tanzania.

 Kamanda wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni Charles Kenyela akifuatilia kwa makini Pambano la ngumi baina ya bondia Mtanzania Thomas Mashali na Mkenya Benard Mackoliech lililofanyika katika ukumbi wa Friends  corner Manzese jijini Dar es Salaam.


Refarii Mark Hatia akimuamuru Thomas Mashali kwenda katika kona yake  baada ya kumwangusha mpinzani wake  Bondia Bernad Mackoliech wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki.

Charles Kenyela akimvisha mkanda wa ubingwa wa Afrika Mashariki na kati Thomas Mashali (Simba Asiyefugika) baada ya kumbwaga mpinzani wake benard Mackoliech.

Kamanda Charles Kenyela katikati aliyeinua mkono juu akiwa na mabondia Thomas Mashali (kulia) Benard Mackoliech (Kushoto) hapa anawaashiria kushikana mikono(fair play) kuonesha kuwa mchezo wa ngumi ni uungwana si uadui.
Baadhi ya Mashabiki waliojitokeza wakishangilia mara baada ya ushindi wa bondia Mtanzania Thomas Mashali dhidi ya Mkenya Benard Mackoliech jana usiku.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top