Latest News


Mkurugenzi wa Sahel Trading Co.Ltd, Ally hazam kushoto akimkabidhi mzani wa kupimia uzito mabondilla 'Ostadhi' mzani huo wenye thamani ya shilingi milioni moja na laki nane umetolewa na kampuni hiyo kutekeleza ahadi yao ya kusaidia mchezo wa masumbwi nchini picha na www.superdboxingcoach.blogspot.coma kwa Yassin Abda

 MAZANI WA KIMATAIFA WA KUPIMIA MABONDIA AMBAPO UNA UWEZO WA KUPIMA UZITO,UREFU, NA KUTAMBUA UJAZO WA MAFUTA YAKO MWILINI YAPO KIASI GANI NA UNAITAJI  UWE NA UZANI KIASI GANI KULINGANA NA UREFU WAKO

Mkurugenzi wa Sahel Trading Co.Ltd, Ally hazam kushoto akimkabidhi mzani wa kupimia uzito mabondia kwa Yassin Abdalla 'Ostadhi' mzani huo wenye thamani ya shilingi milioni moja na laki nane umetolewa na kampuni hiyo kutekeleza ahadi yao ya kusaidia mchezo wa masumbwi nchini picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


NA MWANDISHI WETU
KAMPUNI ya  Sahel Trading Co.Ltd kupitia kwa mkurugenzi wake Ally Hazam  wametoa mzani wa kupimia mabondia kwa kiwango cha hali ya juu kwa ajili ya kuondoa ubabaishaji wa upimaji uzito kwa mabondia

Akizungumza wakati wa kukabidhi mzani huo wenye thamani ya shilingi milioni moja na laki nane  Hazam amesema wameamua kutoa mzani wakitegemea ngumi ndio mchezo pekee ambao unaweza kuliletea sifa taifa kwa haraka zaidi.

Naye Yassini Abdalla 'Ostadhi' aliyepokea mzani huo ambao utakuwa ukitumika kwa mabondia kupima uzito hususani katika mapambano ya kimataifa ameishukuru kampuni hiyo kwa kutoa mzani ahadi ambayo walikuwa nayo muda mrefu lakini leo 'jana' ndio wameitekeleza 

Siku zote dunia nzima cha kwanza kabla mabondia awajapanda ulingoni kwanza wanapima uzito na afya ndio mpambano una endelea. Bila uzani kujulikana hakuna ngumi maana mnaweza kupiganisha mabondia wenye uzani tofauti kitu ambacho akikubaliki dunia nzima

Hivyo sina budi kuishukuru kampuni ya Sahel Trading Co. Ltd kwa kunipatia uzani huu.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top