BARCELONA  NA BAYERN MUNICH VITANI   LEO ULAYA


 Barca wakitoka vichwa chini
 Barca wakiwa mazoezini

Waswahili wana msemo wao usemao “Mwenzako akinyolewa zako tia maji”, Madrid safari yao imefikia tamati Jumanne usiku  huku wakiathiriwa na matokeo ya mchezo wa kwanza, watani zao wa jadi, FC Barcelona nao leo wanapambana na miamba ya Ujerumani FC Bayern Munich katika dimba la Camp Nou huku Barca wakiwa na kumbukumbu ya kutandikwa mabao 4-0  Allianz Arena huko jijini Munich.

 FCBarcelona wanahitaji magoli 5 – 0. Na endapo watashinda magoli 4 – 0  mechi itaongezwa dakika 30 kama mshindi wa jumla hatapatikana changamoto ya mikwaju ya penati itaamua timu itakayosonga hatua ya fainali itakayopigwa katika dimba la Wembley huko jijini London Uingereza.

Mshindi wa jumla wa mechi hiyo nusu fainali  baina ya FC Barcelona na Bayern Munich atakutana na Borussia Dortmund timu ambayo imekata tiketi kwa kuwafurusha mabingwa wa mara TISA wa michuano ya ligi ya Mabingwa Ulaya Real Madrid.

REAL MADRID YATUPWA NJE ULAYA, LICHA YA USHINDI WA 2 – 0

Karim Benzema akifunga bao
Sergio Ramos akishangilia bao alilofunga

Kocha Jose Mourinho akipagawa wakati wa mechi
  Borussia Dortmund wakishangilia ushindi

 Licha ya Real Madrid ya Hispania kuibuka na ushindi wa magoli 2 – 0 dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani timu hiyo imetupwa nje ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya katika mechi iliyochezwa katika dimba la Santiago Bernabeu jijini Madrid.

Matokeo hayo yameitupa nje Real Madrid kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza nchini ujerumani ambapo Mourinho alipiga kipigo cha mbwa mwizi cha mabao 4-1 na baada ya kushinda JANA kwa mabao mawili Madrid wanatoka kwa wastani wa mabao 4-3.

Miamba hiyo ya Hispania ilikuwa inahitaji kufunga magoli 3 – 0 ili iweze kutinga fainali walau kwa faida ya goli la ugenini lakini magoli hayakuweza kuwatoa kimasomaso

Mshindi wa mechi baina ya FC Barcelona na Bayern Munich atakutana na Borussia Dortmund timu ambayo imekata tiketi kwa kuwafurusha mabingwa wa mara TISA wa michuano ya ligi ya Mabingwa Ulaya Real Madrid.

Ilikuwa mechi ngumu kwa vijana wa Mourinho kwani walilazimika kumaliza kipindi cha kwanza wakiwa 0-0 na kipindi cha pili kilipoanza bado mambo yalikuwa magumu mpaka dakika ya 83 ambapo waliandika bao la kwanza kupitia kwa Mfaransa Karim Benzema akipokea pasi nzuri kutoka kwa Mjerumani Mesut Ozil.

Na katika dakika ya 88 beki machachari Sergio Ramos alimalizia pasi maridhawa ya Karim Benzema na kuzamisha gozi kambani, hata hivyo matokeo hayo hayakufua dafu kufuatia kipigo cha 4-1 ugenini.

Katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo Real Madrid walicheza vizuri zaidi ya wapinzani wao lakini walishindwa kupangua ngome imara ya Kocha Flopp aliyetamba toka awali kuwa hawataweza kuwafunga, lakini kipindi cha pili waliachia na kufungwa, kama Madrid wangekuwa makini wangewatoa  baada ya kupoteza nafasi muhimu.

Ozil hatasaulika kwa mashabiki wa soka wa Real Madrid baada ya kupoteza nafasi muhimu za kufunga mabao ambayo yangewapeleka dimba la taifa la Wembley nchini Uingereza kucheza mchezo wa fainali.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top