Kituo
cha sheria na haki za binadam (LHRC) kimezindua ripoti ya kumi na moja ya mwaka
2012 ya uchunguzi juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu na changamoto zilizojitokeza.
Ripoti
hiyo imebainisha tathmini katika mambo mbalimbali likiwemo suala la uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini,
kupinga unyanyasaji wanaofanyiwa baadhi ya wamiliki wa vyombo vya
habari, kuandika habari kwa maslahi binafsi au jamii, kuteswa, kutishiwa maisha na
kuuwawa kwa aliyekuwa mwandishi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten Daud Mwangosi .
Katika
tukio la kuuwawa kwa Daud Mwangosi ripoti hiyo imefanya tathmini na kubaini
kuwa, uhusiano baina ya ya polisi na waandishi wa habari mkoani Iringa si wa
kuridhisha, na kueleza matukio kadhaa ya kunyanyaswa kwa waandishi wa habari .
Mambo
mengine yaliyobainishwa ni pamoja na elimu, afya na haki ya kuishi ambapo kwa
mujibu wa ripoti ya haki za binadamu kwa mwaka 2012 , jumla ya watu 31 wameuawa
na vyombo vya dola huku taarifa hiyo pia ikionyesha bado wananchi wanachukua
sheria mkononi katika utatuzi wa migogoro kadhaa.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment