Waislam wametakiwa kuwekeza katika elimu na kununua ardhi kwa maendeleo na ustawi wa jamii ya sasa na vizazi vijavyo.
 
Hayo yamesemwa na Sheikh Darwesh Kimicha wakati wa kipindi maalum cha dini ya Kiislam cha Redio Mlimani  ambapo amesema kuna umuhimu wa kununua ardhi maalum kwa ajili ya matumizi mbalimbali na kuachana na  utegemezi.
 
Sheikh Darwesh amesema kuwa kama jumuiya za kiislam zitanunua ardhi itakuwa rahisi kwao kujenga shule,misikiti,viwanja na kumbi maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli mbalimbali za kiislam  zikiwemo sherehe na maadhimisho mengine.
 
Katika suala la elimu amesema kuwa waislam wanatakiwa kujiendeleza katika ngazi mbalimbali za kitaaluma na kutobweteka na maendeleo kidogo waliyo nayo 
 
Amesema ni wajibu wa waislam kuweka mfumo thabiti wa kutoa taaluma ya elimu anuwai ikiwemo elimu ya ufundi kwa vijana mbalimbali wa kiislam na kuhakikisha maendeleo yanawafikia.
 
Sheikh Darwesh amesema ameanzisha mipango ya kuwasaidia vijana  zaidi ya 50 eneo la Kibiti Rufiji kwa ajili ya taaluma mbalimbali za kiufundi ili waweze kupambana na ukali wa maisha.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top