Abiria mmoja (mwenye tisheti nyeupe) aliyekuwa akisubiria daladala katika kituo cha mabasi cha mwenge Dar es Salaam akizozana na kondakta na mpiga debe baada ya kukataa kulipisha basi linalofanya safari kati ya mwenge na Posta,aliwagomea akidai basi haliruhusiwi kupanda juu ya vikingo vya barabara kwa madai ni sehemu ya abiria kusimama. Mara nyingi madereva katika kituo hicho wanakatiza licha ya kutotakiwa kufanya hivyo.

Hatimaye kondakta na mpiga debe wakamburuta abiria huyo na kumuweka pembeni ili kuruhusu gari lao kupita kwenye kingo za barabara kinyume cha sheria.

Ajali Nyingine
 Baadhi ya ajali ni za kujitakia angalia ajali ya bodaboda,waendesha pikipiki hao waligongana mara baada ya dereva aliyetoka upande wa kushoto kuchukua mikate kuingia barabara kuu bila tahadhari katika barabara ya Mabatini maeneo ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Ukiwa mjasiriamali tambua fursa hapa picha zinaonekana zinauzwa ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo wahusika walipigwa wakiwa kwenye mkutano mkuu wa wakaguzi wa hesabu za serikali,wanalazimika kukomboa picha moja kwa kati ya shilingi elfu tatu na elfu tano ingawa baadhi walilalamika kuwa walipigwa bila ya ridhaa hivyo kulazimika kuongeza bajeti. Picha nyingi malipo zaidi.

Nani alikwambia siasa haina uhusiano na biashara? hapa ni nje ya hotel Blue Pearl mkutano wa CHADEMA ulikuwa ukiendelea  kufanyika ndani lakini nje kuna vijana wanauza bidhaa mbalimbali zenye nembo ya chama kama vile fulana,kofia, Skafu,mashati,DVD,CD na kadhalika.

Biashara ni popote,vijana wakiwa wamehamishia biashara zao nje ya chuo cha kodi,maeneo ya Mwenge jijini wakati wa shughuli za mahafali zilizofanyika hivi karibuni,kama wanavyoonekana vijana wanauza mashada ya maua,mapambo mengine muhimu kwa shughuli kama hiyo.

Kama kuna kero inayowasumbua wakazi wa jiji la Dar es Salaam ni uwepo wa kunguru weusi maarufu kunguru wa Zanzibar,katika kukabiliana na hilo baadhi ya wakazi na taasisi wanaweka mitego kama inayooneka kwenye picha ili kuwanasa kunguru hao kwa kuwawekea vivutio ndani kama mabaki ya chakula kwa kawaida wakiingia hawawezi kutoka katika mtego huu.Hapa ni chuo cha cha biashara CBE.
Kunguru wa Zanzibar sio waoga kama wale wa bara wenye baka jeupe huwa wana uwezo wa kukwapua kitu kama vile andazi ama mnofu wa nyama ama kipande cha samaki na kuondoka nacho.
Shuhuda mmoja mkazi wa Tandale jijini Dar es Salaam anasimulia kuwa aliwahi kupigana na mke mwenzake baada ya kunguru kuhamisha nguo ya ndani kutoka kwake mpaka bafu la mwanamke mwenzake huyo hivyo wakalihusisha na ushirikina hata hivyo wanafunzi waliomuona kunguru akifanya vituko hivyo walisaidia kutanzua mgogoro huo vinginevyo ingekuwa balaa.
Picha na Gervas Charles Mwatebela 
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top