| Mratibu wa mtandao wa katiba initiative akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha maoni ya Jamii za wafugaji |
| Baadhi ya wawakilishi wa mtandao wa Katiba initiative unaopigania haki za wafugaji wakiwa nje ya jengo la Tume ya Mabadiliko ya katiba mara baada ya kuwasilisha mapendekezo yao. |
Jumuiya
ya wafugaji imetoa mapendekezo ya kutaka masuala ya ardhi na rasilimali
za nchi yanatakiwa kuwekwa katika katiba mpya ijayo ili kuepusha
migongano inayojitokeza mara kwa mara katika jamii.
Mratibu
wa Mtandao wa katiba initiative WILLIAM OLE NASHA
amesema rasilimali ardhi,mali asili na rasilimali watu zinatakiwa kutumika
ipasavyo kwa mustakabali wa maendeleo ya wananchi wote badala ya kuwanufaisha
watu wachache.
Mratibu
huyo amesema miongoni mwa vitu wanavyotaka ni kuhakikisha kuwa mgawanya na
matumizi ardhi unawekwa kikatiba na kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima
pamoja na
Mratibu
huyo amesema wafugaji wamekuwa wakitoa mchango mkubwa wa maendeleo tangu taifa
la Tanzania kujipatia uhuru lakini kila wakati wamejikuta wakinyanyaswa kwa
kuhamishwa kila wanapoweka makazi.
Baadhi
ya wawakilishi wa makundi ya wafugaji wamesema wanataka kuona rasilimali kama
rasilimali asili kama misitu,madini na mbuga za wanyama zinawafaidisha pia
wenyeji wanaoishi kuyazunguka maeneo ya yenye vivutio vya utalii.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment