![]() |
| Waziri Wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa |
Ili kurahisisha zoezi la usambazaji/ugawaji wa hundi hizi kwa wahusika na kupata mrejesho wa haraka wa malipo hayo. Utaratibu ufuatao utafuatwa;
1. Hundi za walimu walio katika Halmashauri za wilaya zitapelekwa kwa Katibu Tawala wa Mikoa husika ili Afisa Elimu wa Mkoa kusaidia kuzipeleka kwa wahusika;
2. Hundi za wakufunzi na walimu walio katika Vyuo vya Ualimu zitapelekwa kwa wakuu wa vyuo vya ualimu husika;
3. Hundi za wakaguzi wa shule wa kanda na wilaya zitapelekwa kwa Mkaguzi Mkuu wa Shule wa Kanda husika.
4. Hundi za madai ya walimu ambayo kwa sasa ni mirathi zitapelekwa kwenye mahakama zilizofunguliwa mirathi hiyo.
Tunashauri wahusika wapewe hundi hizo ndani ya mwezi mmoja toka tarehe zilipopokelewa. Kwa hundi ambazo wahusika hawatakuwa wemejitokeza ndani ya mwezi mmoja ni vyema zikarejeshwa kwa katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Kwa maelezo ya ziada, tafadhali wasiliana na Mhasibu Mkuu wa Wizara kwa namba za simu +255 22 2126828.
IMETOLEWA NA
KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
10/01/2013
Chanzo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:
Post a Comment