Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi Bwana James Mbatia

Wakati makundi mbalimbali yanatoa maoni ya katiba mpya,chama cha NCCR Mageuzi kimependekeza kuwa Lugha ya Kiswahili inatakiwa kutumika katika sekta muhimu zote za mawasiliano.

Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi  bwana James Mbatia alisema lugha ya Kiswahili inatakiwa kuthaminiwa na kuandikwa katika katiba mpya,sheria za nchi ziandikwe kwa kiingereza na mahakama kuu ziitumie kama lugha ya mawasiliano katika utendaji wake.

Mwenyekiti huyo aliwataka watanzania kuachana na kasumba na mtazamo potofu wa kupenda kujifunza na kuona lugha za kigeni ndiyo bora na kudharau Kiswahili ambayo ndiyo sehemu ya utamaduni wao.

Bwana Mbatia alisema inashangaza kuona Wataalam kutoka Kenya wakipata fursa mbalimbali za ajira kupitia lugha ya Kiswahili wakati Watanzania wakishindwa kuzipata licha ya kujivunia kuwa ni lugha ya Taifa.

Imeelezwa kuwa nchi nyingi zilizopiga hatua kimaendeleo zimekuwa zikitumia lugha za asili katika mawasiliano hivyo jitihada za makusudi zinahitajika kukiendeleza zaidi Kiswahili.
 
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top