Serikali imesema inafanyia marekebisho  sheria kandamizi ili kuleta usawa katika jamii  ili kupata mwelekeo wa pamoja katika masuala ya jinsia.

Akifungua semina ya maboresho ya sekta ya sheria  kwa watumishi wa idara mbalimbali za sheria,Waziri wa katiba na Sheria Mathias Chikawe amesema kuwa kuna umuhimu wa sheria ambazo hazifai kwa sasa zifanyiwe marekebisho kwa ustawi wa jinsia zote katika jamii.

Naye Mshauri wa Wanyinda Phillip Katto amesema kuwa suala la usawa wa kijinsia katika jamii ni suala la mchakato wa muda mrefu kutokana tamaduni mila na desturi zilizopitwa na wakati ambazo zilimfanya mwanamke kushindwa kumiliki ardhi.

Mshauri huyo amesema baadhi ya vipengele vya sheria ya ndoa ni miongoni mwa sheria kandamizi dhidi ya mwanamke na utu wake hivyo kuhitajika mabadiliko makubwa ya kisheria. TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top