Jukwaa
la wahariri limetoa mapendekezo kuwa suala la uhuru wa vyombo vya habari
ni suala la msingi ambalo linatakiwa kupewa kipaumbele katika katiba mpya kwa
ustawi wa tasnia ya habari.
Mhariri
Mtendaji wa gazeti la Jamhuri ,ambaye ni Mmoja wa wakilishi wa Jukwaa hilo
Deodatus Balile amesema uhuru wa vyombo vya habari utaifanya tasnia ya habari
kutokandamizwa wala kutoshitakiwa kwa kesi ambazo hazina mantiki.
Bwana
Balile amesema sheria nyingine ambayo kimsingi ni muhimu kwa jamii ni kuhusiana
na haki ya kujieleza na kupata habari pasipo vikwazo vyovyote ili kumuwezesha
mtu yeyote kupata ama kutoa habari kwa mujibu wa katiba.
Wakati
vyombo vya habari vikizidi kuongezeka kila uchao,bado kuna sheria ambazo
zimekuwa zikilalamikiwa kila uchao kudaiwa kuminya uhuru wa vyombo hivyo
ikiwemo sheria ya magazeti ya mwaka 19
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment