Rais Jakaya Mrisho Kikwete

RAIS Jakaya Kikwete hii leo  ameongoza kikao cha wakuu wa nchi tatu zinazounda Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika TROIKA kinachofanyika  jijini Dar es salaam

Kikao hicho pamoja na mambo mengine kitajadili maendeleo ya hali ya siasa nchini Madagascar na hali ya usalama Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo .

Viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria kikao hicho ni Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Troika, Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top