Kikosi Cha timu ya Taifa Stars |
Timu
ya taifa ya Tanzania ya mpira wa miguu Taifa Stars inataraji kushuka ugani saa
11.30 kwa saa za Afrika ya Mashariki katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Mechi
hiyo ya kirafiki dhidi ya Ethiopia ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mchujo
dhidi ya Morocco kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014.
Mechi hiyo itachezwa Machi mwaka huu.
Mechi hiyo itakuwa kipimo cha mwisho kwa
Ethiopia kabla ya kwenda Afrika Kusini kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya
Afrika (AFCON) zitakazoanza Januari 19 mwaka huu.
Ethiopia
iko kundi C pamoja na mabingwa watetezi Zambia, Nigeria na Burkina Faso.
Ethiopia itacheza mechi yake ya kwanza Januari 21 mwaka huu dhidi ya Zambia.
Katika
mechi yake ya mwisho, Taifa Stars iliifunga Zambia bao 1-0 katika mchezo wa
kirafiki uliofanyika Desemba 22 mwaka jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi
hiyo ya kirafiki dhidi ya Ethiopia ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mchujo
dhidi ya Morocco kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014.
Mechi hiyo itachezwa Machi mwaka huu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment