Katibu Mkuu Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Joyce Ndalichako |
Watahiniwa wa mtihani wa kidato
cha sita 2013 watafanya mtihani wa kuhitimu masomo yao mwezi Februari mwaka huu. Hii ni
tofauti na ilivyotangazwa katika mabadiliko ya mihula yaliyofanywa na Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambapo walipaswa kufanya mitihani yao mwezi Mei. Hii ni kwa mujibu wa taarifa za Baraza la
Mitihani Tanzania (NECTA) katika mtandao wao.
Baraza hilo
linasisitiza kuwa mabadiliko hayo hayawahusu watahiniwa wa mtihani kidato cha
sita mwaka 2013.
“Mabadiliko ya mihula yaliyofanywa
na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi yataanza kutumika kwa Watahiniwa wa
Kidato cha Nne mwaka 2013, ambao watafanya mtihani wao mwezi Novemba na
Watahiniwa wa Kidato cha Sita mwaka 2014 ambao watafanya mtihani wao mwezi Mei” inasema taarifa hiyo.
0 comments:
Post a Comment