ROONEY KUIKOSA LIVERPOOL
Wayne Rooney |
Mshambuliaji nyota wa klabu
ya Manchester United Wayne Rooney ataikosa mechi dhidi ya mahasimu wao
Liverpool katika mechi ya ligi kuu kutokana na maumivu ya goti yanayomsumbua.
Kocha wa timu hiyo Sir Alex
Ferguson amethibitisha kuwa kwamba mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza
atakuwa fiti zaidi kwa mechi ya jumatano dhidi ya West Ham United.
Hata hivyo kocha huyo
amefarijika kwa kiasi fulani kutokana na kurejea kwa Anderson na Luis Nani
waliokuwa majeruhi hivyo wataikaribisha Liverpool siku ya jumapili katika uwanja wa
Old Trafford,jijini Manchester .
Wakati wa Man United
wakiwakaribisha mahasimu wao wakiongoza ligi kuu (pointi 52) kwa tofauti ya
pointi 21 dhidi ya Liverpool ambao wako nafasi ya 8 kwa pointi zao 31.
DIEGO MILITO KUREJEA DIMBANI
Diego Milito |
Mshambuliaji mkongwe wa
Inter Milan ya Italia anataraji kurejea
dimbani wikiendi hii baada ya kupona majeraha ya goti yaliyokuwa yakimsumbua.
Milito (33) mshambuliaji wa
kimataifa wa Argentina anataraji kukipiga katika mechi ya leo ligi kuu nchini
Italia serie A dhidi ya Pescara.
Inter Milan bado inapambana
kuhakikisha inarejesha heshima msimu huu kwani mpaka hivi sasa ipo nafasi ya
tano ikiwa na pointi 35,pointi TISA nyuma ya vinara wa ligi hiyo Juventus wenye
pointi 44.
via….supersport.com
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment