Waombaji waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2014/2015 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa tarehe 06/10/2014. Fomu za maelekezo (Joining Instructions) zitatolewa na chuo husika na zitatumwa kwa waliochaguliwa tu. Waliochaguliwa wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yaliyoainishwa kwenye fomu ya kujiunga na Chuo. Aidha, fomu hizi zinapatikana pia kwenye Tovuti ya Wizara:www.moe.go.tz; NACTE:www.nacte.go.tz; na TAMISEMI: www.pmoralg.go.tz

Muhimu:

1. Waombaji waliochaguliwa ni wale wenye ufaulu wa Daraja la I hadi III

2. Waliochaguliwa wanatakiwa kuwasilisha Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA (CSEE na ACSEE) na vyeti vya kuhitimu Elimu ya Sekondari na Mafunzo ya Ualimu.

3. Ada ya mafunzo Stashahada ya Juu ni 600,000/= kwa mwaka (Muhula wa kwanza 300,000/= na muhula wa pili 300,000/=)

4. Wanafunzi watakaosajiliwa Chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SIYO vinginevyo, waweza pata orodha hyo kwa kufungua kiunganishi kimoja wapo hapo chini au kwa kutembelea mfumo wenye majina - bonyeza hapa

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU SAYANSI & HISABATI
MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU ELIMU MAALUMU
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU LUGHA (KISWAHILI, ENGLISH & FRENCH)

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA AWALI
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA MICHEZO
MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA MSINGI
NACTE
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top