Abu Qatada alikabiliwa na tuhuma za kupanga njama ya mashambulizi ya kigaidi nchini Jordan
Mahakama nchini Jordan haijampata na hatia ya tuhuma za kigaidi Mhubiri wa kiisilamu anayesemekana kuhubiri itikadi kali Abu Qatada.

Jopo la majaji wa kiraia waliokuwa katika mahakama hiyo, hawakumpata na hatia yoyote bwana Qatada kutokana na madai kuwa alihusika na njama iliyotibuliwa ya kushambulia sherehe za mwishoni mwa mwaka 2000.

Uamuzi huo umetolewa baada ya Abu Qatada kutopatikana na hatia mwezi Juni katika kosa lengine la kupanga njama ya mashambulizi mwaka 1998 nchini Jordan.

Abu Qatada alitimuliwa kutoka Uingereza mwezi Julai mwaka 2013 kwa madai ya kueneza itikadi kali.
BBCSwahili
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top