Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS lenye nambari za usajili T 677 CYC lililokuwa likitoka Musoma kuelekea Kilari Mkoani Mara likiwa limeumia vibaya sana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi lingine la Kampuni ya MWANZA COACH lenye nambari za usajili T 736 AWJ katika eneo la SabaSaba,Mjini Musoma mchana huu.Watu 36 wamepoteza maisha papo hapo na wengika kujeruhiwa vibaya sana.
 

Kwa mujibu wa Ripota wetu aliyekuwa eneo la tukio inaelezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Basi la J4 ambalo lilikuwa likijaribu kuipita gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK katika sehemu ambayo mbele kuna daraja linaloweza kupitisha gari moja kwa wakati huo.

Kutokana na kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo kasi liliweza kuisukuma kwa ubavuni gari hiyo ndogo ambayo haikuweza kuhimili nguvu ya Basi hilo na kutoka kwenye njia na kwenda kuingia mtoni.

hali iliyoipelekea basi hiyo kuamini kuwa itawahi kupita katika daraja hilo bila kufahamu kuwa Basi lingine linalokuja mbele nalo liko kwenye mwendo kasi huku nalo likitaka kuwahi kupita kwenye daraja hilo.

Ndani ya gari hiyo ndogo kulikuwa na watu watatu, ambapo wawili wamefariki na mmoja amejeruhiwa. Picha na Ahmad Michuzi, Musoma..

Basi la Kampuni ya MWANZA COACH lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS.
Hali ilikuwa hivi katika eneo la tukio lililotokea ajali ya mabasi kupaata ajali baada ya kigongana.

Umati wa Watu ukiwa umekusanyika kwenye eneo hilo ilikotokea ajali hiyo mbaya na kusababisha watu 36 kupoteza maisha pamoja hapo.wakishuhudia tukio hilo la ajali. Gari likiwa ndani ya mto baada ya kutokea ajali.

Guldoza likifanya kazi ya kuichomoa gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye namba ya usajili T 332 AKK lililoshukumwa na basi hilo mpaka kuingia mtoni.Gari hii ilikuwa na watu watatu, ambapo wawili wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa.

Sehemu ya waokoaji waliofika kwenye tukio hilo.

Wanausalama wakijadiliana jambo kwenye eneo hilo la tukio.

Baadhi ya Mizigo ya abiria wa mabasi hayo wakiwepo waliopoteza maisha.

Hivi ndivyo uokozi namna ulivyokuwa ukiendelea baada ya ajali kutokea.

Askari Polisi wakitoa miili ya watu wawili waliokuwemo kwenye gari hiyo.

MATUKIO YA AWALI YA AJALI HIYO ILIYOTOKEA MKOA WA MUSOMA NA ZAIDI YA ABIRIA 36 KUPOTEZA MAISHA.

Mabasi hayo yakiwa yamegongana 
Baadhi ya miili iliyofariki katika ajali hiyo.




Basi la Jumanne lililokuwa linatoka Sirari kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi la Mwanza coach lililokuwa linatoka Mwanza kwenda Musoma. Ajali imetokea katika eneo la daraja la sabasaba.

Wajanja wa Town TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top