Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinal Pengo

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinal Pengo amesema shughuli za mchakato wa Katiba zifanyike kwa amani na kwamba ziwalinde Watanzania katika umoja na mshikamano waliyokuwa nao.

Pia, amewataka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuweka masilahi yao kando na kutanguliza masilahi ya taifa kwa faida ya Watanzania.

Akizungumza jana kwenye uzinduzi wa Katisa Katoliki Magomeni, Kardnali Pendo alisema ni vyema viongozi wakafahamu kwamba Watanzania ni watu wanaopenda amani, na kwamba yeye angepAenda kuona amani iliyopo inadumu.

Alisema: "Niseme kwamba, shughuli za mchakato wa kuandika Katiba Mpya zifanyike kwa amani."

Aliongeza: "Ni vyema tukatambua kuwa Watanzania ni wapenda amani, hivyo wasingependa kuona kukijitokeza tofauti kati ya wajumbe wa Bunge hilo,"

Alisema kama tunataka nia ni kupata katiba bora, ni lazima wajumbe wabunge la Maalum la Katiba kuweka masilahi yao kando na kuangalia yale ya taifa kwa faida ya Watanzania wote.

Alitoa mfano kwa baadhi ya vingozi wa nje ya nchi wanavyotambua mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kuwa ni mtu aliyependa amani, umoja na mshikamamno.

Alisema leo (jana) alifuatilia vyombo vya habari na kusikia kuwa Rais wa Zimbabwe (Robert Mugabe) akimuelezea Mwalimu Nyerere kama kiongozi shupavu aliyeweka misingi ya amani Tanzania kwa kuwa alikuwa mpenda amani.

Naye, Paroko wa Kanisa hilo Joseph Matumaini alisema Kanisa hilo limejengwa kwa ghalama ya Sh1.25 bilioni fedha ambazo zimetokana na michango ya waumini wao.

Alisema: "Kanisa hili limejengwa kwa jitihada za waumi kwa kujitolea, na kwamba tunawashukuru wote kwa kuijenga nyumba ya mungu,"
Alisema Kanisa hilo lina uwezo wa kuchukua waumini 1500.
Chanzo, mwananchi
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top