Posho Bunge la Katiba yaundiwa tume  
SAKATA la nyongeza ya posho limechukua sura mpya baada ya Mwenyekiti wa muda wa Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Ameir Kificho, kuunda kamati ya watu sita kulishughulikia.
 
Kificho alisema kamati hiyo italishughulikia jambo hilo na kuishauri serikali namna bora ya kulifanya ili wajumbe waifanye kazi kwa ufanisi zaidi.

Juzi wajumbe wa Bunge hilo walikuwa wakipinga kiwango cha posho ya  sh 300,000 wanazopewa kwa siku, wakitaka walipwe sh 500,000 au sh 700,000 kwa madai kuwa gharama za maisha mjini Dodoma zimepanda.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top