Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe
ZIPO
sababu na vipo visingizio. Visingizio ni vitu au ni mambo yale ambayo
tunayalaumu ili tu kukwepa kukilaumu kile hasa kinachohusika na matatizo
yetu.
Kwa mfano, mtu akiambiwa kuwa barabara anayotaka kuitumia ina
miiba mikali na yeye akaamua kuendelea kuifuata, akichomwa na miiba
anaweza kuchagua kulaumu kisingizio au sababu.
Kisingizio
ni rahisi sana kwani anaweza kusema amechomwa na miiba kwa sababu viatu
vyake vilikuwa laini sana na hivyo miiba ikapenya – na ni kweli
inawezekana viatu ni laini na ni kweli miiba imepenya. Lakini sababu
hasa ni kuwa hakusikiliza maonyo na hakujiandaa ipasavyo.
Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambacho ni kipenzi na chaguo la
mamilioni ya watu wanaotaka mabadiliko mazuri ya kisiasa nchini,
kinakabiliwa na uchaguzi wa kuamua kutafuta visingizio au kutafuta
sababu ya kwanini kinapata shida kushinda chaguzi hizi ndogo na
kinahitaji kutumia nguvu kubwa sana kushinda viti vichache sana.
Matokeo
ya chaguzi za udiwani zilizofanyika Jumapili yameonyesha kuwa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kimeendelea kuwa kizingiti (kisiki labda ni neno zuri
zaidi) cha upinzani Tanzania kwani bado hakijaonyesha dalili ambazo
tunahubiriwa kila siku kuwa kiko tayari kuondoka madarakani.
CHADEMA na tatizo la kupendwa
Nimewahi kuandika mara kadhaa huko nyuma, lakini ifae kurudia tena hapa; CHADEMA inasumbuliwa na tatizo la kupendwa sana. Katika huku kupendwa haitaki kujiangalia kama imevaa nguo nzuri au la; haitaki kuangalia kama vipodozi vinaendana na rangi ya ngozi yake au hata kama rangi ya midomo imevaa vizuri au imeenda hadi mashavuni!
Nimewahi kuandika mara kadhaa huko nyuma, lakini ifae kurudia tena hapa; CHADEMA inasumbuliwa na tatizo la kupendwa sana. Katika huku kupendwa haitaki kujiangalia kama imevaa nguo nzuri au la; haitaki kuangalia kama vipodozi vinaendana na rangi ya ngozi yake au hata kama rangi ya midomo imevaa vizuri au imeenda hadi mashavuni!
Ukijua
kuwa unapendwa au unapendeka unaweza kujikuta unaanza kunata; kuringa au
kujiona. Unajiona kuwa wewe ndio wewe hakuna mwingine na kuwa
wanaokusema ama wanakuonea wivu au hawawezi kujipara kama wewe!
Katika
kufanya hivyo mtu hajioni makosa yake na ukichelewa sana hata watu
ambao walikuwa marafiki hawakuonyi tena wanakuacha tu huende kujiaibisha
mwenyewe hadi siku ile picha yako itokee kwenye gazeti moja la udaku
umesaula kama popo kwenye paa la pango! Ukijiona mzuri usishangae watu
wakakuacha udhurike!
CHADEMA inapendwa na hili halina shaka; wapo
watu wanaipenda kiasi cha kutoa mali na hali zao kuitetea na
kuipigania. Wapo wenye kuipenda kiasi cha kufa; na wapo waliokufa kwa
ajili ya CHADEMA au katika mazingira ya kukitetea chama.
Maelfu
kama siyo mamilioni ya Watanzania wanaiona CHADEMA kama mkombozi wao na
wanaiona kama chama mbadala wa CCM na ni kwa sababu hiyo matokeo ya
uchaguzi huu mdogo uliopita yamewagusa watu hawa si kwa namna ya
kufurahisha au kufariji; yamewaacha na maswali ambayo bado hawajayapatia
majibu yake.
CHADEMA isifiche kichwa kama mbuni
Jambo baya zaidi katika kutafuta visingizio ni kujaribu kujifanya huoni tatizo au hutaki kuliona tatizo. Mbuni ni ndege mwenye umbo kubwa, lakini pia mwenye kichwa kidogo ukilinganisha na umbo lake. Fikiria mbuni ajaribu kujificha kwa kuchomeka kichwa mchangani au nyuma ya kijiti akiamini kuwa haonekani.
Jambo baya zaidi katika kutafuta visingizio ni kujaribu kujifanya huoni tatizo au hutaki kuliona tatizo. Mbuni ni ndege mwenye umbo kubwa, lakini pia mwenye kichwa kidogo ukilinganisha na umbo lake. Fikiria mbuni ajaribu kujificha kwa kuchomeka kichwa mchangani au nyuma ya kijiti akiamini kuwa haonekani.
Kufanya hivi ni kutokuwa mkweli
kwa sababu alichofanya ni kujificha yeye asione siyo yeye asionekane. Ni
kwa sababu hiyo msemo wa kutokuficha kichwa mchangani upo; kwamba kuna
wakati inabidi tuwe tayari kuuona ukweli na tusijizibe wenyewe kuona kwa
kudhani hatuonekani.
CHADEMA inapaswa kukubali kosa lake kubwa
ambalo limeendelea kuwasumbua sasa, na kwa muda mrefu sasa wamekuwa kama
mbuni na kichwa mchangani. Wakati umefika wauone ukweli.
Visingizio hivi si vya kweli
Maelezo ambayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara kuelezea kutokufanya vizuri zaidi kwa CHADEMA au kuhalalisha kuwa wamefanya vizuri kulinganisha na huko nyuma yamepitwa na wakati kwani hayatoshi kuelezea kwanini CCM bado inatamalaki! Baadhi ya maelezo ambayo tumeyasikia huko nyuma na yanatolewa tena hivi sasa ni haya:
Maelezo ambayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara kuelezea kutokufanya vizuri zaidi kwa CHADEMA au kuhalalisha kuwa wamefanya vizuri kulinganisha na huko nyuma yamepitwa na wakati kwani hayatoshi kuelezea kwanini CCM bado inatamalaki! Baadhi ya maelezo ambayo tumeyasikia huko nyuma na yanatolewa tena hivi sasa ni haya:
CCM inatumia nguvu za
dola kuminya upinzani, watu wanauza shahada zao, Tume ya Uchaguzi
inapendelea CCM, Daftari la Wapiga Kura halijaboreshwa hivyo wanachama
na mashabiki wengi wa CHADEMA hawapigi kura, CCM wameshinda kwenye kata
zao na wao ndio wamepoteza zaidi kuliko CHADEMA.
Hivi ndivyo
visingizio vikubwa vya kufanya vibaya kwa CHADEMA au kutokufanya vizuri
zaidi kama ilivyotarajiwa au kuaminiwa. Ninaposema ni visingizio sitaki
kueleweka kuwa navipuuzia kuwa havina maana au si vya kweli; la hasha.
Ninachosema
hasa ni kuwa hizi siyo sababu hasa za kwanini CHADEMA inashindwa
kuigaragaza CCM na kuwapa furaha wanachama na mashabiki wake badala ya
kushinda sehemu ambazo watu walitarajia itashinda au kufanya mgaragazo
(upset) moja kama ya Njombe. Sasa tukikubali hoja hizi tunakubali
visingizio na hivyo tutakuwa tunasubiri tena maelezo kama haya Chalinze
na Kalenga!
Kosa kuu la CHADEMA
Binafsi naamini kosa kubwa la CHADEMA kuhusiana na hizi chaguzi ndogo ndogo lilifanywa kabla ya uchaguzi wa 2010 na limeendelea kufanywa baada ya uchaguzi ule uliolitetemesha taifa na kutikisa ngome za CCM. Kosa hili ni CHADEMA kukubali kwenda kwenye uchaguzi chini ya tume ile ile, sheria zile zile, mfumo ule ule wa uchaguzi! Kosa hili linatokana na CHADEMA kuamini katika wema wa CCM na hisani ya serikali kuwa yumkini wataweka mazingira mazuri ya kuusaidia upinzani ushinde! Hili ni kosa kubwa zaidi la kimkakati na litaendelea kuwang’ata CHADEMA kwenye makalio hadi watakapolikubali na kulisahihisha.
Binafsi naamini kosa kubwa la CHADEMA kuhusiana na hizi chaguzi ndogo ndogo lilifanywa kabla ya uchaguzi wa 2010 na limeendelea kufanywa baada ya uchaguzi ule uliolitetemesha taifa na kutikisa ngome za CCM. Kosa hili ni CHADEMA kukubali kwenda kwenye uchaguzi chini ya tume ile ile, sheria zile zile, mfumo ule ule wa uchaguzi! Kosa hili linatokana na CHADEMA kuamini katika wema wa CCM na hisani ya serikali kuwa yumkini wataweka mazingira mazuri ya kuusaidia upinzani ushinde! Hili ni kosa kubwa zaidi la kimkakati na litaendelea kuwang’ata CHADEMA kwenye makalio hadi watakapolikubali na kulisahihisha.
Kitendo cha CHADEMA kuendelea
kukubali kushiriki chaguzi hizi chini ya sheria zile zile mbovu
(zisizoweka utaratibu mzuri wa kusimamia uchaguzi, au kuandikisha wapiga
kura) na mfumo ule ule (wenye kupendelea CCM) ni kukubali matokeo yake!
Nimewahi
kuandika huko nyuma – nafikiri ilikuwa wakati wa uchaguzi wa Arumeru
Mashariki na hata ule wa Kiteto – kuwa CHADEMA inapokubali kuingia
uwanjani huku inajua sheria za mchezo ni mbovu, refa amenunuliwa, na
hakuna uwezekano wa “fair play” basi inakuwa imekubali na matokeo!
Ndiyo
maana kwenye michezo mingine watu wanagomea kabisa kwenda uwanjani kwa
sababu hawaamini kuwa mchezo utakuwa huru na wa haki kwa pande zote.
Uchaguzi wa Tanzania tayari umethibitisha kuwa hauwezi kuwa wa haki na
huru kwa kadiri ya kwamba mfumo wetu haujajengwa katika kutetea haki za
raia! Unaweza vipi kuwa na uchaguzi ambao watu hawaandikishwi kupiga
kura?
Hili ni kosa kubwa; haya yote ambayo nimeyaita ni
visingizio ni matokeo tu ya kosa hili! Kwa kukubali kuendelea kushiriki
chaguzi hizi chini ya mfumo na sheria hizi mbovu CHADEMA inapoteza haki
ya kulalamika!
Kitu cha kwanza ambacho wengi tulikiona kabla ya
uchaguzi wa 2010 ni kuwa mvuto wa Dk. Slaa ulishtua sana CCM kiasi
kwamba kama watu wangekuwa wanaruhusiwa kujiandikisha kupiga kura wakati
wa kampeni, matokeo yangekuwa tofauti sana. Mfumo wetu wa kujiandikisha
kupiga kura ni lazima ubadilishwe.
Baada ya uchaguzi ule,
nilitarajia – na niliandika hili kwa kina – kuwa CHADEMA wangepigania
kuhakikisha kuwa mfumo wa kuandikisha watu kupiga kura ungebadilishwa;
mojawapo ni kulifutilia hili ‘daftari la wapiga kura’ la kitaifa!
Sioni mantiki kwanini kuwe na daftari moja (kwa maana ya kuwa orodha moja inayosimamiwa na tume). Kwanini watu wasiandikishwe kupiga kura kwenye halmashauri zao? Kuna ubaya gani kuwa na mfumo unaoruhusu watu kujiandikisha kupiga kura muda wowote wa mwaka na kuwa endapo uchaguzi unatokea basi majina yaliyoko kwenye orodha hiyo kwa kipindi cha siku thelathini zilizopita ndiyo yatatumika badala ya miaka kama ilivyo sasa!
Hivi
hili kweli tunahitaji ma-genius kutoka Uingereza kuja kutusaidia kuona
linafanyika? Hivi mbona hili halina gharama kubwa ya hivyo?
Siyo
tu kupigania suala la uandikishwaji, lakini Sheria ya Uchaguzi na Tume
ya Uchaguzi vilitakiwa kufanyiwa mabadiliko. Badala yake ndugu zetu
CHADEMA wakakubali kanyaboya la “Katiba Mpya” ambalo liliwazuia
kupigania mabadiliko mengine kwani mambo yote wameambiwa “kwenye Katiba
Mpya”.
Kila mtu akitaka kutoa wazo wanaambiwa “subirini Katiba Mpya” wakati sote tunajua kuwa katiba mpya isipopita katiba ya sasa itatumika na kimsingi mifumo ya sasa itatumika! Lakini CHADEMA wamekubali!
Sasa wafanye nini?
Binafsi nina mapendekezo machache tu ya kuwasaidia ndugu zetu hawa, kama wanaweza kusaidika kwa kweli.
Binafsi nina mapendekezo machache tu ya kuwasaidia ndugu zetu hawa, kama wanaweza kusaidika kwa kweli.
Mosi,
ni kutangaza kutoshiriki uchaguzi wa Kalenga na Chalinze kama Tume ya
Uchaguzi haitowapatia wananchi wa huko haki ya kujiandikisha kupiga
kura, wale ambao hawajaandikishwa.
Hoja kuwa ati wakijitoa CCM watapita ni hoja isiyo na msingi; tayari majimbo hayo yalikuwa ya CCM na kama wakiyarudisha basi wayarudishe huku wakijua kuwa wamewaburuza watu. Kukubali kushiriki ni kukubali matokeo yake na kwa kweli kutumia gharama zisizo za lazima.
Pili, kuweka shinikizo kwa Tume ya
Uchaguzi kubadilisha utaratibu wake wa kuboresha daftari la wapiga kura
na kutaka utumike mfumo mzuri wa kuliboresha katika vipindi vinne vya
mwaka (yaani kila baada ya miezi mitatu).
Hii ina maana kuwa mtu
yeyote ambaye anataka kujiandikisha kupiga kura au kubadilisha taarifa
zake anaweza kufanya hivyo wakati wowote ndani ya miezi mitatu kabla
daftari halijaboreshwa (updated) katika robo ile ya mwaka. Hii ina maana
ya kuwa daftari la wapiga kura litakuwa la wakati mno kuliko ilivyo
sasa.
Tatu, CHADEMA ifikirie sana juu ya namna ya kuwashawishi watu ambao si wana-CHADEMA au wapinzani kupigia kura wagombea wake. Hili ni jambo la muhimu sana kwa sababu tunakoelekea tofauti ya ushindi itakuwa si kwa wanachama na mashabiki kupigia kura chama bali kwa wale wasio wanachama na wasio mashabiki kushawishiwa kupiga kura.
Kwa mfano,
katika kata nyingi inaonekana bado CHADEMA haijaweza kuwashawishi watu
wengi zaidi wasio CHADEMA kupigia kura. Kwanini? Hili linahitaji
kufanyiwa utafiti kidogo.
Nne, CHADEMA isidharau ukweli mmoja ambao labda wapinzani na wale wapenda mabadiliko wakati mwingine hatuamini kuwa ni kweli; CCM ina watu wenye kuipenda na wanaipenda kweli kweli. Hili nitaliangalia kidogo kwa kina wiki ijayo, In Shaa Allah.
Wakati
mwingine katika kufikiria tunapendwa sana tunajisahau kuwa wapo wengine
ambao nao wanapendwa. Labda tunafikiri tunapendwa kwa sababu tunatoka
nadhifu sana, mkwanja wa nguvu na ujiko wa kila namna, na katika
mazingira hayo tunasahau kuwa labda wengine wanapendwa pia kwa sababu
nyingine!
Kudhania kuwa watu wengi wanaichukia CCM ni kutokuwa
wakweli kwa sababu matokeo lukuki yanaonyesha kuwa CCM bado inapendwa na
watu na wengine hata kama hawakubaliani nayo sana, lakini bado wako
tayari kuipa kura yao kuliko kupeleka upinzani; hili nalo linahitaji
jibu: kwanini?
Kwanini wapo watu, tena wengine maskini kabisa, na
wamechoka hadi ulimi, lakini watu hao hao wenye kulalamikia shule,
maji, elimu, afya wakipewa nafasi kuchagua bado wanaichagua CCM?
Kwanini? CHADEMA isipuuzie hili jibu na hawa ndio watu ambao inatakiwa
itafute mbinu ya kisasa ya kuwafikia kwani ndio tofauti ya kushindwa na
kushinda!
Ni matumaini yangu kuwa hoja yangu itazua mjadala na
kuona kama kweli visingizio vinavyotolewa vinatosha na kama sababu
niliyoisema mimi ina ukweli wake au na mimi natafuta visingizio tu ila
sababu yenyewe nimeikwepa pia. Au na msomaji anatafuta kisingizio cha
kwanini sababu yangu siyo ya kweli!? Heri ya Mwaka Mpya kwa wasomaji
wangu!
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment