
Kiongozi wa Hong Kong amesema kuwa Uchina haitabadilisha kanuni za uchaguzi
Kiongozi wa jiji la Hong Kong C Y
Leung ametoa wito wa kusitishwa maandamano ambayo amesema yamedumaza
shughuli katika jiji zima.
Amesema kuwa maandamano hayo hayawezi kubadili msimamo wa China juu ya mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Raia wa HK wakiwasha taa za simu zao usiku
Bwana Leung pia amekataa kuitikia wito wa kujiuzulu kwak ekutoka kwa vuguvugu lililopanga maandamano hayo.

Raia wamekataa kuondoka mabarabarani wakitaka mabadiliko katika sera za uchaguzi
Wakati huo huo Marekani imesema inafuatilia kwa karibu kinachoendelea Hong Kong na imeutaka utawala kuchukua hatua.
Katika
mkutano wa wanahabari msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest amesema
Marekani inaunga mkono matakwa ya watu wa Hong Kong.

Raia wa Hong Kong wakivurumushiwa moshi
Makumi kwa mamia ya
waandamanaji wa Hong Kong wanaendelea na maandamano yao kwa siku
nyingine tena baada ya kudhoofisha maeneo muhimu ya jiji hilo wakati wa
mchana.

Maandamano hayo yamebandikwa jina maandamano ya miavuli.
Waandamanaji hao sasa wanamtaka Mkuu wa utawala wa Hong Kong Leung Chun-Ying ajiuzulu..
Wakati huo huo Marekani imesema inafuatilia kwa karibu kinachoendelea Hong Kong na imeutaka utawala kuchukua hatua.

Raia wa Hong Kong akijiandaa kwa makabiliano na polisi
Katika mkutano wa wanahabari
msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest amesema Marekani inaunga mkono
matakwa ya watu wa Hong Kong.

Waandamani wamebandika karatasi zenye ujumbe kwenye mabasi ya umma HK
"Duniani kote, na hii ni kweli
katika Hong Kong na maeneo mengine, Marekani inaunga mkono kimataifa,
uhuru, kama vile uhuru wa kukutana kwa amani na uhuru wa kujieleza.

Maelfu ya waandamanaji katika barabara za Hong kong
Marekani inautaka utawala wa Hong Kong kuchukua hatua, na kwa upande wa waandamanaji kutoa maoni yao kwa amani"
BBC
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment