JESHI   la polisi  Mkoani Ruvuma  linawashikilia  wanakijiji zaidi ya kumi na tano  (15) wakiwemo  Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, mwenyekiti wa Serikali  ya kijiji cha Ntunduwalo, Afisa  mtendaji wa kijiji hicho na  Afisa  Mtendaji wa Kata ya Rwanda kufuatia  wanakijiji cha  Ntunduwalo kuzuia  magari  yanayokwenda na kutoka yakiwa  yamesheheni Mkaa  ya Mawe toka kwenye Mgodi wa Mngaka wilayani Mbinga ambako   polisi wamelazimika kutumia  mabomu  ya machozi kuwatawanya  wakati wakizuia magari yaliyobeba  makaa ya mawe mpaka  walipwe  fedha  za fidia  wanazodai.
 
Habari  zilizopatikana jana mchana Mjini Songea ambazo zimezibitishwa na  kamanda  wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deudedit  Nsimeki zimesema  kuwa tukio hilo lilianza  kutokea  juzi  majira  ya saa  za asubuhi ambako  wananchi  wa kijiji cha Ntunduwalo walijipanga  na kufunga  barabara inayokwenda kwenye mgodi wa makaa ya  mawe uliopo karibu na kijiji  hicho.
 
Alisema  wanakijiji  hao  walikuwa  na lengo la kuishinikiza  serikali ili iwalipe nyongeza ya fidia  ambayo  wanadai  kuwa hapo awali walipunjwa wakati wanafanyiwa  tasmini ya mali zao  zilizokuwepo ndani ya maeneo yaliyochukuliwa  na mgodi huo kwamba serikali ilitumia sheria  ya zamani badara  ya sheria  iliyopo hivi sasa  ambayo inaonesha  kuwa ni kubwa.
 
Alifafanua  kuwa  kundi kubwa la  wananchi wakiwemo watoto  na akina mama waliokuwa  wamekaa mbele lililojipanga ni lile  lililolipwa mwanzo  kwa kutumia  sheria ya uthamini ya zamani  ambapo wanadai kuwa  wamekuwa  wakiahidiwa mara kwa mara  na serikali  kuwa  watalipwa kiasi cha fedha cha  fidia  kilichobaki.
 
Alieleza  zaidi kuwa kutokana na hali hiyo wanakijiji hao waliamua  kuchukua  uwamuzi wa kuzuia shughuli za magari yanayobeba  makaa ya mawe yasiingie kuchukua makaa  ya mawe iwala  kutoka  kwenye  eneo hilo.
 
Alibainisha zaidi kuwa  kufuatia kuwepo kwa vurugu hiyo iliyosababisha  shughuli za mgodi  kusimama  polisi baada ya kupewa taarifa hiyo walikwenda kwenye  kijiji hicho  wakiwa  wameongozana  na katibu tawaa  wa wilaya ya Mbinga  Idd  Mponda ili kujaribu  kuongea  na wananchi, kuwasii  waondoe kizuizi hicho  ili magari  yaendelee na kazi ya kusomba  makaa  yam awe lakini wananchi walikataa na walimueleza  katibu tawala huyo kuwa  hawamuitaji kumuona yeye pamoja na watu wengine wala  Mkuu  wa wilaya hiyo kuwasikiliza  wanachotaka  walipwe fedha  zao wanazodai na si vinginevyo.
 
Aliongeza  kusema kuwa  mvutano huo wa mazungumzo kati ya katibu tawala  wa wilaya  hiyo  Mponda  na wanakijiji yalidumu kwa muda mrefu hadi juzi  majira  ya saa tatu  usiku polisi waliamua  kulilinda  eneo hilo na baadaye  walifanikiwa  kuwakamata watu watano  ambao  wanadaiwa  kuwa  ndio waliokuwa  viongozi wa vurugu hizo.
 
Amewataja baadhi ya wanashikiliwa  kuwa ni Mwenyekiti wa serikali ya kijiji  cha  Ntunduwalo  John  Nyimbo  (36), Matrida  Nchimbi  ( 49) ambaye  ni Afisa mtendaji wa kata ya Rwanda, Joachim Ngaponda ambaye  ni Afisa  mtendaji wa kijiji hicho, mwenyekiti wa kamati ya miradi  ya  kijiji hicho Garusi Komba  (49)  na  John  Joachim Mahai  (45) mkazi wa kijiji cha Malindindo  tarafa  ya Mbuji wote  wanaendelea  kuhojiwa  na Polisi.
 
Aidha,  Kamanda  Nsimeki alisema kuwa  pamoja  na polisi  kuwashikiria wanakijiji hao jana majira ya asubuhi vurugu  zilirejea  tena  ambapo  polisi  walilazimika   kutumia  mabomu ya  machozi kuwatawanya  wanakijiji  hao ambao  waliendelea  kuyazuia  magari yaliyokuwa yamebeba makaa  ya mawe  huku  wananchi  wakijitahidi  kuyazuia  yasipite.
 
Hata hivyo  jitihada  za songeayetu kumpata mwenyekiti  wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mbinga ambaye pia  ni mkuu wa wilaya  hiyo  Senyi  Ngaga  ziligonga  mwamba  baada  ya kupigiwa  simu kwa zaidi ya mara tatu ambayo haikuweza kupokelewa  na  baadaye  alipopigiwa simu mara ya nne ilipokelewa  na mtu mwingine ambaye alidai kuwa DC  yupo kwenye  kikao hivyo hana nafasi ya kuongea  muda huo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top