Serikali imesema ujenzi wa viwanda katika mikoa ya Lindi na Mtwara utasaidia kukuza shughuli za maendeleo ya shughuli za kiuchumi katika maeneo hayo.
Waziri wa nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa kuanzishwa na kujengwa kwa bomba la gesi asili nchini ni faida badala ya kutumia mafuta ya taa na mkaa.
Akizungumza wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo ya nishati na madini Prof. Muhongo amesema kuanzishwa kwa mradi wa gesi asilia kutasaidia kukuza pato la taifa .
Hata hivyo kambi lasmi ya upinzani kupitia Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA Mh.John Mnyika , ameiomba serikali iahilishe utandazwaji wa bomba la gesi asili ili wananchi waelimishwe na kuhakikisha mikataba yote juu ya gesi na iwekwe wazi kwa wananchi ili kuepusha vurugu.
Wakati wa bajeti hiyo ya wizara ya nishati na madini ikiwekwa mezani mambo kadhaa yanatarajia kuibuliwa katika miradi ya gesi asilia ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa viwanda, kuongezeka kwa ajira pamoja na kukua kwa uchumi wa nchi.
Hivi karibuni wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara waliandamana wakipinga kujengwa kwa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, kitu kilichofafanuliwa na waziri Mhongo kama ni changamoto ambayo yaweza kukwamisha mchakato wa kutekeleza miradi ya maendeleo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Waziri wa nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa kuanzishwa na kujengwa kwa bomba la gesi asili nchini ni faida badala ya kutumia mafuta ya taa na mkaa.
Akizungumza wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo ya nishati na madini Prof. Muhongo amesema kuanzishwa kwa mradi wa gesi asilia kutasaidia kukuza pato la taifa .
Hata hivyo kambi lasmi ya upinzani kupitia Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA Mh.John Mnyika , ameiomba serikali iahilishe utandazwaji wa bomba la gesi asili ili wananchi waelimishwe na kuhakikisha mikataba yote juu ya gesi na iwekwe wazi kwa wananchi ili kuepusha vurugu.
Wakati wa bajeti hiyo ya wizara ya nishati na madini ikiwekwa mezani mambo kadhaa yanatarajia kuibuliwa katika miradi ya gesi asilia ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa viwanda, kuongezeka kwa ajira pamoja na kukua kwa uchumi wa nchi.
Hivi karibuni wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara waliandamana wakipinga kujengwa kwa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, kitu kilichofafanuliwa na waziri Mhongo kama ni changamoto ambayo yaweza kukwamisha mchakato wa kutekeleza miradi ya maendeleo.

0 comments:
Post a Comment