Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemwandikia Spika wa Bunge barua ikimtaka Waziri wa Nishati na Madini aeleze sababu za kutoa leseni ya uchimbaji Uranium Wilayani Namtumbo kinyume na sheria.
Yafuatayo ni maelezo ya Mheshimiwa Zitto yaliyopatikana katika ukurasa wake wa facebook
Nimeandika barua Kwa Spika wa Bunge kutaka Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo Bungeni kuhusu uamuzi wake wa kuwapa leseni kubwa ya kuchimba Uranium huko wilayani Namtumbo. Mnamo tarehe 10 Agosti 2012 Waziri alitamka ndani ya Bunge "sisi tunajua zaidi ya anavyojua yeye, Leseni haijatolewa na haitatolewa mpaka Kampuni ya Mantra Resources ilipe kodi". 
Kodi ya ongezeko la mtaji (capital gains tax) ya $189m kufuatia mauzo ya mradi wa #Mkuju River Project kutoka kampuni ya Mantra kwenda kampuni ya AMRZ ya Urusi iligomewa kulipwa. 
TRA wamepeleka shauri hilo mahakama ya kodi na mpaka sasa maamuzi hayajatolewa. 
Kwa mujibu wa mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2012, kabla ya Waziri mwenye dhamana ya madini kubariki mauzo ya kampuni, anapaswa kupata Kibali Cha kwamba kodi zote stahili zimelipwa. 
Kibali Kwa kampuni ya mantra kilitolewa bila kujali hitaji la kisheria na sasa kampuni hii imepewa leseni. 
Maamuzi haya ya Waziri wa Nishati na Madini yanalikosesha Taifa mapato ya zaidi ya Tshs 300 bilioni ambazo zingeweza kumaliza tatizo la nyumba za walimu nchi nzima na kulipia madai yote ya walimu. 
Fedha hizi zingeweza kujenga barabara ya lami kutoka Manyoni mpaka Itigi. 
Fedha zingeweza kukarabati reli ya Kati na kuirejesha katika ubora wa unaotakiwa. 
Kwa mujibu wa kanuni za Bunge nimetaka Waziri atoe maelezo bungeni na wabunge wajadili. Ni dhahiri kwamba serikali inayoongozwa na CCM imeamua kumaliza utajiri wote wa nchi na kuugawa kwa wageni Kwa bei ya che. 
 Wananchi Ni lazima kusimama imara kukataa uporaji huu na maamuzi haya ya kiburi Cha kudharau Bunge yaliyoyafanywa na Serikali.
Via FB 
 
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top