Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba
Tume ya mabadiliko ya katiba nchini imewataka watanzania kukubali na kupokea maamuzi magumu yatakayotolewa na tume hiyo wakati wa kutoa rasimu ya uundwaji wa katiba mpya kwa wananchi ambayo inatarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwezi juni mwaka huu.
Akitoa taarifa ya tathimini ya kazi mbalimbali ya tume ya mabadiliko ya katiba ya uundwaaji wa mabaraza ya katiba ya wilaya na serikali za mitaa, mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Joseph Sinde Warioba amesema kuwa tume iko tayari kufanya maamuzi magumu na kuwaomba wananchi nao kuwa tayari.
Jaji Warioba amesema katika zoezi hilo, tume imekabiliana na changamoto kadhaa zikiwemo za vitendo vya rushwa, udini na siasa lakini akasisitiza kuwa kuwa katiba itakayotengenezwa itakuwa ya
watanzania wote na si ya kikundi flani.
watanzania wote na si ya kikundi flani.
Tathimini ya tume hiyo inaonyesha kuwa asilimia 99.8 ya kata zote za Tanzania bara zimepitiwa katika uundwaji wa mabaraza ya katiba huku asilimia 96.4 ya shehia visiwani Zanzibar zikifanikiwa kuunda mabaraza.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment