Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amewaagiza watendaji wote kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi na kuwapatia raia wa Tanzania vitambulisho vinavyowahusu huku akiongeza kama watakiuka sheria na taratibu watavuruga zoezi kuna hatari ya watu wasio raia kuvipata vitambulisho visivyowahusu.

Mheshimiwa Rais amesema kwa wale watakaobainika kutoa taaarifa za upotoshi kwa lengo la kuficha ukweli kwa makusudi hatua stahiki za kinidhamu na kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Akizindua  mfumo wa utambuzi na usajili vitambulisho vya Taifa jijini Dar es Salaam Rais Kikwete amewataka Watanzania kushirikiana na mamlaka ya vitambulisho ya Taifa NIDA kwa maendeleo ya Taifa.

Rais Kikwete amesema watanzania wanatakiwa kujitokeza na kutoa taarifa sahihi ili kufanikisha zoezi la uandikishaji na uhakiki wa taarifa za watu wote ili kufikia mwaka 2015 watanzania wote wapate vitambulisho hivyo.

Rais Kikwete amesema ukosefu wa fedha kuwa changamoto kubwa katika zoezi la utengenezaji wa vitambulisho vya Taifa ni gharama kubwa hivyo serikali inafanya jitihada  za makusudi kuhakikisha watu wote wanakuwa na vitambulisho hivyo kwa kuvigharamia

Rais amesema kama serikali itajitahidi kutoa ushirikiano kwa mamlaka ya vitambulisho ya Taifa NIDA kuhakikisha inaondoa na kupunguza changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo ikiwemo upungufu wa rasilimali watu na uhaba wa fedha.

Dakta Kikwete amesema kuwa lengo ni kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 Watanzania watumie vitambulisho hivyo wakati wa uchaguzi huo.

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Dakta Emmanuel Nchimbi amesema tayari NIDA imeshampata mkandarasi na vituo vya  kutunzia taarifa za elektroniki  na kupata michoro ya ujenzi wa ofisi za wilaya.

Akiongea katika uzinduzi wa mradi  huo mkurugenzi  mkuu wa nida Bwana Dickson Maimu   amesema kuna changamoto kubwa ya fedha na rasilimali watu hivyo kumuomba Rais kuisadia mamlaka yake kulifanyia ufumbuzi suala hilo.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top