Jeshi la polisi Mkoa wa Kinondoni linawashikilia watuhumiwa 7 kwa tuhuma za kuingia nchini isivyo halali, kuwapokea na kuwahifadhi raia wa kigeni isivyo halali na kujihusisha na biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu[Human Trafficking].

Kamanda wa polisi mkoa huo Charles Kenyela amesema tukio hilo limetokea huko kimara Bonyokwa nyumbani kwa ISSA  OMARY, kufuatia taarifa toka kwa wasiri wa polisi zilizoelezea kwamba raia wa kigeni wasiofahamika walikuwa wamehifadhiwa katika makazi yake.

Amesema  Jeshi la Polisi lilipofuatilia taarifa hizo  kwa kufanya upekuzi nyumbani kwake, mtuhumiwa huyo alitoroka na mara baada ya upekuzi  watu wanne[4]raia wa ETHIOPIA walipatikana wakiwa wamefungiwa kwenye chumba kimoja ndani ya nyumba hiyo

Katika mahojiana ya awali, watuhumiwa hao walieleza kwamba walitokea nchini Ethiopia kupitia mpaka wa Tanzania hadi Dar es salaam ambako wangesafirishwa kuelekea Afrika Kusini kupitia mpaka wa Mtwara.

Kamanda Kenyela ameongeza kuwa siku moja baada ya kukamatwa kwa wahamiaji hao, jeshi la polisi lilifanikiwa kumnasa mmiliki wa nyumba hiyo na kuwataja wafanyabiashara wawili raia wa Burundi kuwa ndio wanaofanya biashara hiyo

Watuhumiwa hao wawili pia walikamatwa kwenye hoteli ya Luch Time Manzese jijini na kwamba taratibu za kuwafikisha mahakami zinafanyika

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top