Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa amewataka wadau wote wa maendeleo ya mkoa wa Mtwara kusitisha harakati zao za maandamano na mihadahara ya kupinga ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwenda Dar es salaam na badala yake kukaa pamoja kujadili suala hilo
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari,imemnukuu rais Mkapa akizitaka pande zote kushirikiana kwa pamoja kupitia historia,kuchambua kwa kina mikakati ya utekelezaji wa mradi huo na kufikia muafaka wa ujio wa maendeleo.
Rais Mkapa amesema fujo, vitisho, kupimana nguvu na malumbano kamwe si masharti ya maendeleo bali mazungumzo yataboresha sera, ya uwekezaji ya mkoa na nchi kwa ujumla.
Amesema vituko na kauli za hivi karibuni kutoka kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa zimekaribia kujenga kutokuelewana kati ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali, kati ya wanachama wa vyama vya siasa na viongozi wao, kati ya wananchi na viongozi wa Serikali.
Ameongeza kuwa Mtafaruku huu haufai kuachwa uendeleee na kutishia usalama kwa kuwa mipango, Mikakati na mbinu za Utekelezaji wa maendeleo siyo siri na kwamba maelezo yake mazuri yanaweza kutolewa yakadhihirisha namna na kasi ambayo raslimali zitawanufaisha wananchi wa eneo hilo. TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment