Yaya Toure.
Gervais Lombe Yao Kouassi (Gervinho).

Klabu za ligi kuu nchini England zitaanza kuonja shubiri ya kuwakosa nyota wake kutoka Afrika ambao wanazitumikia timu zao za Taifa katika michuano ya mataifa Afrika huko Afrika Kusini.

Tembo wa Afrika, Ivory Coast inaonekana ni timu ya taifa ambayo itaziathiri timu nyingi za ligi kuu nchini England kwani ina wachezaji wengi zaidi kuliko nchi nyingine zinazoshiriki michuano hiyo.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Manchester City wataanza kuzikosa huduma za Yaya na kaka yake Kolo Toure ambao wanaitumikia Ivory Coast huko bondeni katika michuano hiyo itakayoanza kutimua vumbi Januari 19 hadi Februari 10 mwaka huu.

Kocha Msaidizi wa Man City David Platt amesema kuwa hawajui Yaya na Kolo Toure watafika hatua gani lakini wanajua jinsi ya kufanya ili kuziba nafasi zao.Suala hili ni sawa na wanapokuwa majeruhi wa muda mrefu tunawakosa uwanjani,lakini wangekuwepo walikuwa muhimu kikosini.Mwaka Yaya Toure hakuwepo kikosini lakini tulichukua ubingwa wa ligi kuu England’’ aliongeza kocha huyo.

Wanaijeria Obi Mikel na Victor Moses watajiunga na Super Eagles na kuachana na kibarua chao Stamford bridge makao makuu ya Chelsea kwa muda kupisha shamrashamra za  michuano ya mataifa ya Afrika.

Newcastle United itamkosa mchezaji wake tegemeo Cheikh Tiote huku Washika bunduki wa London Arsenal wakimkosa mchezaji Gervinho ambaye anakwenda kuitumikia Ivoryo Coast inayoshiriki katika michuano hiyo katika kundi D la Algeria,Tunisia na Togo.

Aruna Kona wa Ivory Coast naye atatengana na klabu yake ya Wigan Athletics kwa ajili ya michuano hiyo yenye msisimko mkubwa barani Afrika.

Naye Kocha wa Morocco Rachid Taoussi Adel amewaita kikosini Taarabt Marouane Chamackh ambaye anaitumikia West Ham kwa mkopo akitokea Arsenal.

Tottenham itamkosa mshambuliaji wake wa kimataifa wa Togo Emmanuel Adebayor, huku kocha Andres Villas Boas akisema wataheshimu uamuzi wa Adebayor kama ataamua kuichezea Togo au kubakia White Hart Lane.

Hata hivyo kukosekana Senegal maarufu kama Simba wa Teranga kunatoa nafuu kwa makocha kama Rafael Benitez wa Chelsea ambaye atamtumia mchezaji wake mpya Demba Ba huku kocha Newcastle akimtumia pacha wake  Papis  Cisse.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top