Serikali imetakiwa kufanya mabadiliko makubwa  ya sheria ya tume ya taifa ya uchaguzi na sheria ya uchaguzi bila kujali mchakato wa mabadiliko ya  katiba
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo  CHADEMA Freeman Mbowe amesema pia kunatakiwa tume huru ya uchaguzi ambayo itafanya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 uwe huru na haki.
Kiongozi huyo amesema kuwa huenda mabadiliko ya katiba yasifanyike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu 2015 hivyo mabadiliko ya sheria zilizopitwa na wakati ni muhimu bila kujali  kukamilika kwa mchakato wa katiba.
Bwana Mbowe amesema mabadiliko ya uchaguzi yasipofanyika kutatoa taswira tofauti hivyo angalizo ni kufanya mabadiliko kwani wananchi wamechoka kuyumbishwa na tume ya uchaguzi ambayo amedai siyo huru.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top