Wadadisi wanasema nchi nyingi za Magharibi mwa Afrika zinakabiliwa na changamoto za miundo msingi.
 
Shirikisho la kimataifa la msalaba mwekundu, limesema kuwa kikundi kingine cha wahudumu wa afya kilishambuliwa Jumanne Kusini Mashariki mwa Guinea walipokuwa wakikusanya miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola.

Mfanyakazi mmoja wa shirika hilo, anauguza majeraha baada ya kujeruhiwa vibaya katika shambulizi hilo katika eneo la Forecariah.

Kwa mujibuwa maelezo ya  mkazi mmoja, jamaa wa wagonjwa waliofariki walianza kuwashambulia wafanyakazi hao sita wa kujitolea, kuwashambulia kwa mawe na kisha kuharibu magari yao.

Huu ni uvamizi wa hivi karibuni dhidi ya wahudumu wa afya ambao bila shaka unakwamisha juhudi za kupambana na ugonjwa huo mkali.

 Wiki jana madaktari wengine na wandishi wa habari walishambuliwa Magharibi mwa nchi hiyo.
BBCSwahili TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top