Viongozi wa kundi la mataifa saba tajiri zaidi duniani, G-7, wanafanya mazungumzo kwa siku ya pili mfululizo hivi leo mjini Hague, Uholanzi ajenda kuu ikiwa ni hatua ya Urusi kunyakua jimbo la Crimea kutoka Urusi.

Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1998, Moscow imenyimwa kiti katika kongamano hilo. Mkutano wa dharura wa G-7 uikubaliana kufutilia mbali kundi la G-8, kundi la mataifa manane tajiri zaidi duniani, ambalo linaishirikisha Urusi.

Viongozi wa mataifa ya kundi hilo wameonya kuwa vikwazo zaidi vitatolewa iwapo Urusi itaingia maeneo ya mashariki au Kusini mwa Ukraine ikiwepo kulenga sekta ya kawi nchini Urusi. Lakini Marekani kadhalika imesisitiza kuwa fursa ya kusuluhisha mzozo huo wa njia ya kidiplomasia ingalipo.
Chanzo: BBC
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top