Viongozi wa kundi la mataifa saba tajiri zaidi
duniani, G-7, wanafanya mazungumzo kwa siku ya pili mfululizo hivi leo
mjini Hague, Uholanzi ajenda kuu ikiwa ni hatua ya Urusi kunyakua jimbo
la Crimea kutoka Urusi.
Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1998, Moscow
imenyimwa kiti katika kongamano hilo. Mkutano wa dharura wa G-7
uikubaliana kufutilia mbali kundi la G-8, kundi la mataifa manane tajiri
zaidi duniani, ambalo linaishirikisha Urusi.
Viongozi wa mataifa ya kundi hilo wameonya kuwa
vikwazo zaidi vitatolewa iwapo Urusi itaingia maeneo ya mashariki au
Kusini mwa Ukraine ikiwepo kulenga sekta ya kawi nchini Urusi. Lakini
Marekani kadhalika imesisitiza kuwa fursa ya kusuluhisha mzozo huo wa
njia ya kidiplomasia ingalipo.
Chanzo: BBC
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment