Washambuliaji ndani ya jumba la Westgate 
Kenya imetoa majina ya wanaume wanne ambao inasema walifanya shambulio dhidi ya jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi majuma mawili yaliyopita ambapo watu zaidi ya 60 waliuwawa.

Wanaume hao walionekana kwenye picha za kamera za usalama zilizopatikana Westgate baada ya jumba hilo kuvamiwa kwa siku nne.

Msemaji wa jeshi aliwataja wanaume hao kuwa Abu Baara al-Sudani, Omar Nabhan, Khattab al-Kene na Umayr ambapo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa. 

Taarifa mjini Nairobi zinaonesha kuwa wawili kati yao wana uhusiano na al-Qaeda na mmoja ana uhusiano na kundi la al-Shabaab ambalo lilisema lilishiriki katika shambulio la Westgate.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top