Zuma akikaribishwa na Mugabe alipozuru Harare zamani 
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametoa zile alizoita, hongera nyingi kwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, ambaye ameshinda muhula wa saba wa uongozi akiwa na umri wa miaka 89.

Mpinzani mkuu wa Bwana Mugabe, Morgan Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 61, amekataa matokeo na amesema atapeleka malalamiko mahakamani.

Viongozi wa mataifa ya magharibi yamesema yana wasi-wasi kama uchaguzi ulikuwa wa halali.

Bwana Mugabe alipata asili-mia-61 ya kura katika uchaguzi wa rais.

Na chama chake cha ZANU-PF kilipata thuluthi mbili ya viti vya bunge.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

1 comments:

Anonymous said... August 4, 2013 at 11:55 PM

Mugabe is a great man.
He knows what it is to be Huru/ Independent.
Afrika is for Afrikans.Zimbabwe is for Afrikans so no whites should dictate to Afrikans how to run their affairs.Bravo Mugabe the Afrikan Hero.
Natamani marais wote wa Afrika wajifunze from Mugabe and Gadafi na Thomas Sankara

 
Top