Waziri wa Afya, DK. Hussein Mwinyi.
Watanzania wametakiwa kujenga utamaduni wa kupima afya za watoto na kupata elimu ya malezi ya watoto hasa walio chini ya miaka mitano kwa ajili ya ukuaji wenye siha njema.
 
Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU jijini Dar es Salaam Dakta Ali Mzige  amewataka wananchi kujitokeza jumapili wiki hii katika hospitali hiyo kwa ajili ya upimaji wa Afya za watoto walio chini ya miaka mitano bila malipo yoyote.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa asilimia 42 ya watoto walio chini ya miaka mitano wamedumaa kutokana na kukosa lishe mahususi kwa ajili ya ukuaji wa miili yao.

Takribani watoto 130 walio chini ya miaka mitano hufariki dunia kila siku hapa nchini kutokana na Utapiamlo yaani lishe duni hivyo kuhitajika jitihada za pamoja katika kukabiliana na tatizo hilo. 

Mkurugenzi huyo amesema watoto wengi wana uzito pungufu,wengine wamekonda na kudumaa kimwili na kiakili kutokana na lishe duni.

Utapiamlo hapa nchini unaiweka Tanzania nafasi ya tatu barani Afrika kwa utapiamlo kutokana na lishe duni,nchi inayoongoza ni Congo DRC ikifuatiwa na Ethiopia.

Cha ajabu hapa nchini  ni kwamba hata mikoa inayozalisha  chakula na matunda kwa wingi pia imeathirika zaidi na ugonjwa wa Utapiamlo. Mikoa hiyo ni  Morogoro, Mbeya,Tanga, Rukwa, Iringa na Manyara.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top