 |
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete
akionekana katika Sare zake za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).Picha hii inatajwa kupigwa Mwanzoni mwa Miaka ya 80 wakati huo Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Jeshini. |
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Anne Simamba Makinda
katika Kivazi chake na Namna alivyotengeneza nywele zake.Picha hii ilipigwa Mwaka 1994 wakati Mama Anne Semamba Makinda akiwa ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Gavana
wa Kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania, Waziri wa Zamani wa Fedha,
Mfanyabiashara na Mkulima Mashuhuri, Mchunga Mbuzi aliyebobea, Fundi
Viatu aliyepata Elimu kwa Msaada wa Chama cha Ushirika, Mwasisi wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA na Mmoja wa Viongozi Madhubuti wa
Taifa hili, Mzee Edwin Mtei.Picha hii ilipigwa Mwezi Aprili Mwaka 1974 wakati Bwana Edwin Mtei alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki.
Pichani
ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Mizengo
Kayanza Peter Pinda (wa Kwanza Kushoto) akiwa pamoja na Mbunge wa
Simanjiro, Bwana Christopher Ole Sendeka (Wa pili kushoto), Aliyekuwa
Mkuu wa Mikoa Mbalimbali hapa Nchini, Bwana Ditopile Ukiwaona Mzuzuri
(wa tatu kushoto) na wa mwanzo upande wa kulia ni Kijana wa Mjini
William Vangimembe Lukuvi.Picha hii ilipigwa Miaka ya 80 wakati huo Vijana hawa wakiwa ni Viongozi wa Jumuia ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment