Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi
(CUF) Taifa, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba
Kufuatia kauli zenye kuudhi kujitokeza mara kwa mara bungeni mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF taifa Profesa Ibrahim Haruna Lipumba amelitaka Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kufuata kanuni na taratibu za kuendesha taasisi hiyo muhimu.
Profesa Lipumba
amesema kutokana na mwenendo wa bunge wa kuzomea hovyo, kutovumiliana kutotii
amri ya spika na wabunge kutohudhuria
bungeni lipumba amesema ni lazima bunge hilo liache ubabe na kutenda haki.
Aidha
mwenyekiti huyo amesema ofisi ya spika ifuate sheria, kanuni na taratibu za bunge ili kujenga misingi ya utawala wa haki na usawa katika
kuliongoza bunge na kupunguza misuguano ya mara kwa mara inayojitokeza baina ya
wabunge wa upinzani na chama tawala.
Kiongozi
huyo amelitaka bunge kujikita katika
kutetea maslahi ya wananchi badala kutawaliwa na lugha ya kejeli na matusi kitu
ambacho amesema hakiwezi kuwasaidia wananchi waliowachagua.
Katika hatua nyingine profesa Lipumba ambaye pia ni
mtaalam wa uchumi ameitaka serikali kusikiliza madai ya wakulima
wa korosho katika wilaya ya Liwale mkoani Lindi ili kuepuka vurugu na machafuko yaliyotokea
mapema Jumatano wiki hii.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment