Spika wa bunge Mh. Anne Makinda

Spika wa bunge Mh. Anne Makinda amelazimika kuahirisha bunge hadi siku ya Jumatatu tarehe 29 ya mwezi wa nne na kuitaka serikali kuiangalia upya bajeti hiyo baada ya wabunge wengi kukataa mapendekezo ya bajeti hiyo iliyowasilishwa na waziri wa maji Profesa Jumanne Maghembe.

Wabunge wengi wametoa maoni yao wakidai bajeti ya wizara hiyo ina  mapungufu mengi yanayopelekea kutokamilishwa  kwa miradi mbalimbali ya maji.

Miongoni mwa mambo yaliyokosolewa na wabunge ni ,ufinyu wa bajeti na uchakavu wa miundo mbinu ya maji hivyo kuwakosesha wananchi huduma hiyo muhimu ya maji .

Aidha wamesema wanaomba serikali kupeleka maji vijijini kwa haraka ili kupunguza kero wanayoipata akina mama na watoto kwenda kutafuta maji umbali mrefu na kuwafanya watumie muda mwingi kwenye kufuatilia maji.

Katika mawasilisho yake waziri mwenye dhamana Prof. Jumanne Maghembe alisema tatizo la maji linachangiwa zaidi na uharibifu wa vyanzo vya maji , ongezeko la idadi ya watu pamoja na uchakavu wa miundombinu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top