JOSE MOURINHO NIKO TAYARI KULAUMIWA TUKITOLEWA
Kocha wa Timu ya Real Madrid, Jose MourinhoKocha Jose
Mourinho amechochea moto kwenye mbio za kuwania fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya kwa kusema kuwa yuko tayari kubeba lawama ikiwa klabu yake ya Real Madrid itatupwa nje ya michuano dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Mechi
hiyo itapigwa usiku wa
leo ambapo Real Madrid inahitaji ushindi wa magoli 3 – 0 ili kutinga
fainali
mara baada ya kuangukia pua baada ya kufungwa magoli 4 – 1 katika mechi
ya
kwanza iliyopigwa Signal Iduna Park huko Ujerumani.
Ushindi wa 4 - 1
mpaka dakika 90 utafanya kuongezwa dakika 30 mshindi asipopatikana
changamoto ya mikwaju ya penati itatumika kuamua mbabe wa kutinga
fainali ya michuano hiyo.Tayari Jose Mourinho kasema katika soka lolote
linawezekana.
Kocha huyo amesema badala ya
wachezaji wake kulaumiwa yeye ndiye anastahili kubeba lawama zote ‘katika soka wadau wengi wanahusika katika
mafanikio ya timu lakini pindi timu hiyo ikifanya vibaya lawama zote anatakiwa
kuzibeba kocha’alisema kocha Mourinho.
Mario Goetze
Robert Lewandovsky
Licha ya tishio la kuondoka
kwa wachezaji wake mahiri Mario Goetze na Robert Lewandovsky,kocha Mourinho
amesema anaamini Dortmund wataendelea kuwa imara na kuwapata wachezaji mbadala
wa nafasi hizo.
Dortmund ilishinda taji la
ligi ya mabingwa Ulaya mwaka 1997 huku Real Madrid ikishinda taji hilo mwaka
2002.
Mahasimu
wa Real Madrid FC
Barcelona watakuwa na kibarua pevu cha kurejesha matumaini ya kutinga
fainali
itakaposhuka ugani siku ya Jumatano usiku dhidi ya Bayern Munich ya
Ujerumani huku
ikiwa na kumbukumbu ya kuchabangwa magoli 4 – 0 katika dimba la Allianz
Arena huko
Munich.
BARCA watahitaji ushindi wa magoli 5 - 0 ili kufuzu fainali
ushindi wa magoli 4 - 0 katika dakika 90 utawapeleka dakika 30 za
nyongeza ikishindikana hapo ni changamoto ya mikwaju ya penati kuamua
mshindi.Lionel Messi na Xavi Hernandez wamekiri ugumu uliopo katika
kubadili matokeo hayo.
NI LIONEL MESSI TU ATAKAYETUBEBA-BARCA
Lionel Mess
Xavi Hernandez
Wakati timu ya Barcelona ya Hispania ikitaraji kushuka ugani siku ya Jumatano
kupambana na Bayern Munich ya Ujerumani katika mechi ya marudiano ligi ya
mabingwa Ulaya imekiri kuwa kutinga fainali kunategemea ubora wa Messi siku
hiyo.
Katika mechi ya awali miamba hiyo ya Catalunya iliambulia kichapo cha
magoli 4 – 0 katika mechi ya kwanza iliyochezwa dimba la Allianz Arena.
Kocha msaidizi wa BARCA Jordi Roura amesema afya ya mchezaji huyo imekuwa
ikiimarika lakini anaamini atakuwa fiti kwa mchezo huo utakaochezwa katika
uwanja wao wa nyumba NOU CAMP.
‘messi ni mchezaji bora duniani hivyo asipokuwepo dimbani utaona tofauti
na akiwepo dimbani utajua utofauti wake’.
Kutokuwa fiti kwa asilimia 100 kwa Messi katika mchezo uliopita dhidi ya
Bayern Munich ni miongoni mwa kinga kwa makocha wa Barcelona kupoteza mechi
hiyo.
BARCA watahitaji ushindi wa magoli 5
- 0 ili kufuzu fainali ushindi wa magoli 4 - 0 katika dakika 90 utawapeleka
dakika 30 za nyongeza ikishindikana hapo ni changamoto ya mikwaju ya penati
kuamua mshindi.
Lionel Messi na Xavi Hernandez wamekiri ugumu uliopo katika
kubadili matokeo hayo.
0 comments:
Post a Comment