Wakulima wa bonde la Mpunga Kiwalani Mlandizi mkoani Pwani wamelalamikia hatua ya halmashauri ya Kibaha Vijijini kuchukua eneo lao bila maridhiano na kulibadilisha matumizi yake.

Mwenyekiti wa umoja wa wakulima hao Rajab Chuma amesema utaratibu wa kuwaondoa katika eneo la Kiwalani haukushirikisha pande zote mbili ili kufikia muafaka kabla ya kubadilisha matumizi ya ardhi ambalo awali lilitumika kwa ajili ya kilimo.

Mwenyekiti huyo amesema chanzo cha mgogoro huo ni mkuu wa shule ya sekondari na halmashauri kutaka kuwahamisha kwa madai kwamba ni wavamizi kitu ambacho kimewashangaza kwani walimiliki maeneo hayo hata kabla ya sekondari kujengwa.

Katibu wa umoja wa wakulima hao Abillahi Rashidi Saad  amesema kuwa wanapanga kwenda mahakamani na kulifikisha suala hilo kwa waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi ili kupata suluhu ya tatizo hilo.

Hata hivyo Mkurugenzi hakuweza kupatikana  ili kutoa ufafanuzi juu ya suala huku  Mkuu wa Shule ya Sekondari Ruvu kutopatikana  kwa madai ya ya kuwa nje ya kituo chake kwa shughuli maalum ya kikazi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top