Naibu waziri wa Mali Asili na Utalii, Lazaro Nyalandu
Watanzania wametakiwa kuendelea kufanya jitihada za makusudi katika kutunza miti ili  uhifadhi wa mazingira kwa  ustawi wa jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Mbao ya miti ulimwenguni,ambayo kitaifa imefanyika jijini Dar es Salaam,Naibu waziri wa Mali Asili na Utalii Lazaro Nyalandu amesema miti ni muhimu kama rasilimali.
Serikali imesema itaendelea kutunza mazingira ya Tanzania kwa kukomesha ukataji miti na misitu bila vibali kwani vitendo hivyo ni kinyume cha sheria.


Naibu Waziri huyo amesema watanzania wanatakiwa kuendelea kupanda na kutunza miti iliyopo kwani husaidia kuleta mvua za kadiri na kuzuia nchi kugeuka Jangwa.


Hata hivyo alizungumzia bidhaa zinazotokana na Mbao amesema kazi za ubunifu kama uchongaji vinyago ni muhimu kama ajira na biashara lakini kwa wahusika wafanye kazi kwa kufuata sheria.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top