Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na  Makamu wa Rais Mstaafu wa Benki ya Dunia, Bwana Justin Yifu Lin, Ijumaa wiki hii Februari mosi, 2013 Ikulu, Dar es Salaam. Kulia  ni Balozi wa China katika Tanzania Mheshimiwa  Lu Youqing.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini baada ya  kuthibitisha maelezo yake binafsi kwenye Fomu ya Kitambulisho cha Taifa wakati alipokamilisha taratibu za kupatiwa Kitambulisho hicho  nyumbani kwake jijini Dar es salaam  leo, Ijumaa, Februari Mosi, 2013. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Bwana Dickson E Maimu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha kwa ajili ya Kitambulisho cha Taifa wakati alipokamilisha taratibu za kupatiwa Kitambulisho cha Taifa nyumbani kwake asubuhi ya jana, Ijumaa, Februari Mosi, 2013.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akichukuliwa alama za vidole wakati alipokamilisha taratibu za kupatiwa Kitambulisho cha Taifa nyumbani kwake asubuhi ya jana, Ijumaa, Februari Mosi, 2013. 

PICHA NA IKULU




TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top