Profesa Anna Tibaijuka akiongea na wanahabari jijini Dar es Salaam kuhusiana na utekelezaji wa ujenzi wa Mji mpya wa Kigamboni, Dar es Salaam
  
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka amewataka viongozi kuwa wazalendo na kuacha kuwapotosha wananchi juu ya uendelezaji mradi wa Kigamboni kwani una umuhimu mkubwa kwa ukuaji wa uchumi wa Watanzania.
Profesa Tibaijuka amesema serikali imejipanga kuhakikisha inatoa elimu kwa umma kuhusiana na manufaa ya kuendeleza eneo la mji mpya wa Kigamboni.
Taarifa iliyotolewa na Wizara hiyo imefafanua kuwa mbali na kutoa elimu kwa wananchi,serikali inatafuta fedha za kutosha kuendeleza mradi na kupima maeneo husika kwa ajili ya kuendeleza mradi huo.
Waziri huyo amesema mji huo utakuwa kitovu cha maendeleo ya kiuchumi kutokana na fursa za uwekezaji na kulifanya jiji la Dar es Salaam kushindana miji mingine duniani.
Profesa Tibaijuka amesema hatua nyingine zinazofanyika ni kufanya tathmini ya mali na kujenga nyumba mpya za kuishi wananchi watakaohamishwa kupisha mradi wa ujenzi wa mji mpya.
Ujenzi wa mji mpya Kigamboni ni mkakati wa serikali kukabiliana na ukuaji wa jiji ambao utakuwa na wakazi laki NNE na uendelezaji huo utafanywa kwa ushirikiano wa serikali na taasisi binafsi.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top