Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.
Hayo yamesemwa na Balozi wa Marekani nchini Alfonso Lenhardt
wakati walipokuwa na mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, Ikulu mjini Zanzibar.
Balozi huyo
alieleza kuwa Marekani inathamini sana uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake
na Zanzibar na kusisitiza kuwa itaendelea kuiunga mkono katika kuhakikisha
miradi ya maendeleo inayoisimamia ukiwemo mradi mkubwa wa umeme inafanikiwa.
Katika maelezo
yake, Balozi huyo alisifu juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar katika kupambana na Malaria pamoja na kuimarisha sekta zake za
maendeleo huku akieleza jinsi hatua zinazochukuliwa na Ubalozi wake katika
kuitangaza Zanzibar nchini mwake kutokana na amani na utulivu uliopo ikiwa ni
miongoni mwa hatua za kuutangaza utalii wa Zanzibar.
Kwa upande wa
mradi wa MCC, Mkurugenzi Mkaazi wa Mradi huo nchini Tanzania Bwana Karl
Fickenscher, alieleza maendeleo yaliofikiwa katika mradi mpya wa
umeme kutoka Ras Kiromoni hadi Fumba ambapo tayari ulazaji waya umeshakamilika
na uwekaji nguzo pamoja na uwekaji waya kutoka Fumba hadi mtoni umefikia hatua
nzuri na kueleza mategemeo ya kazi za mradi huo kumalizika mwishoni mwa mwezi
ujao.
Naye Rais Shein kwa upande wake alimueleza Balozi
huyo pamoja na ujumbe aliofuatana nao kuwa Zanzibar inathamini sana ushirikiano
kati yake na Marekani pamoja na juhudi zake za kuunga mkono miradi ya Zanzibar.
0 comments:
Post a Comment