Imeelezwa kuwa misingi ya haki za binadamu inaweza kutekelezwa endapo tu nchi husika itafuata mfumo wa utawala bora ambao utakuwa unatoa haki kwa kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali.
Kauli hiyo imetolewa na mhadhiri wa sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, James jesse wakati wa mkutano wa kufanya tathmini mapendekezo yaliyotolewa wadau kuhusiana na masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu.
Bwana Jesse amekiri bado kuna changamoto katika suala la kumiliki mali hususan ardhi kwa mwaanchi wa kawaida hivyo ameitaka serikali kuwashirikisha wananchi katika masuala yote ya kumiliki rasilimali za taifa kwani hilo ni jukumu la serikali yoyote duniani.
Katika hatua nyingine mhadhiri huyo wa chuo kikuu cha dare s salaam, amekanusha kuwa misingi ya haki za binadamu haiwezi kutekelezeka kwani kuna nchi nyingi ambazo zimeweza kuheshimu na kutekeleza kwa vitendo haki za binadamu kwa wananchi wake.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top