Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Tanzania na
Ufaransa zimekubaliana kuwa na mpango mwingine wa miaka mitatu ambako Ufaransa itasaidia
maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwamo ya huduma ya kijamii ikiwamo
ile ya upatikanaji kwa maji safi na salama.
Hayo yamefikiwa
katika mazungumzo kati ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika
la Maendeleo ya Kimataifa la Ufaransa (AFD) Bwana DovZerah mjini Paris, Ufaransa
ambako Rais Kikwete amemaliza ziara yake
rasmi ya Kiserikali ya siku tatu.
Aidha,
nchi hizo mbili zimekubaliana kuwa makubaliano hayo mapya yalenge katika kuelekeza
nguvu na raslimali hizo za maendeleo katika sekta chache, mbili ama tatu, ili raslimali
hizo ziweze kutumika vizuri na matokeo yake kuonekana badala ya kusambaza raslimali
hizo kwa sekta na maeneo mengi.
Mara
baada ya kumshukuru Bwana DovZerah kwa mchango mkubwa wa Ufaransa katika mpango
wa maendeleo wa miaka mitatu kati ya 2006 na 2010, Rais Kikwete amependekeza kuanzishwa
kwa mpango mpya, jambo ambalo Mkurugenzi Mkuu huyo amelikubali mara moja.
Rais Kikwete
pia amependekeza kuwa raslimali katika mpango huo mpya zielekezwe katika sekta na
maeneo machache, mawili ama matatu, ili raslimali hizo ziweze kutumika kwa mafanikio
makubwa zaidi na matokeo yaonekane waziwazi.
Chini ya mpango
wa kwanza ambako Ufaransa iliipatia Tanzania kiasi cha
dola za Marekani 50.9 nguvu zilielekezwa katika kusaidia upatikanaji wa maji safi
na salama katika miji ya Utete na Mpwapwa na katika miji midogo inayozunguka Ziwa
Victoria.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment