SALUM HARUNA MSONGELE NI MMOJA WA WAFANYAKAZI WA WALIOACHISHWA KAZI KINYUME CHA SHERIA AMEITUMIKIA KAMPUNI  YA KOBIL TANZANIA HIYO KWA MIAKA 11 
RAMADHANI KIDAWEMBA PIA ALIKUWA MFANYAKAZI WA KOBIL TANZANIA KWA MIAKA 10
CHRISTINA PAUL KIBOMA
 Baadhi wa waliokuwa wafanyakazi wa kampuni ya mafuta ya KOBIL TANZANIA wameiomba serikali kuwasaidia kupata haki zao baada ya kuachishwa kazi kinyume cha sheria .

Wakiongea katika mahojiano maalum wawakilishi wa wafanyakazi hao wamedai waliachishwa kazi ghafla kwa madai ya kampuni yao kuyumba na kushindwa kujiendesha hivyo kuamua kupunguza wafanyakazi 12 kati ya  43.

Wawakilishi hao Christina Paul Kiboma,Salum Haruna Msongele na Ramadhani Kidawemba wamesema kuwa wanachopinga ni kunyanyaswa na kuachishwa kazi kinyume cha sheria pasipo mawasiliano ya awali na kuamriwa kuondoka ndani ya dakika 10 tu.

Baadhi ya wafanyakazi waliopunguzwa kazini walinyang’anywa vifaa binafsi na akaunti zao kufungwa mara  baada ya kuachishwa kazi hivyo kuwaomba wanaharakati za binadamu kuingilia kati na kuwatetea na kunyanyaswa uongozi wa kampuni hiyo.

Jitihada za kumpata kaimu mkurugenzi wa kampuni hiyo bwana Paul Mkato zinaendelea.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

 
Top