![]() |
Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania John Tendwa |
Vyama vya siasa vimetakiwa kujipanga vyema kwa ajili ya
uchaguzi ili kupata matokeo mazuri katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na ule wa
serikali za mitaa mwaka 2014.
Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema
viongozi wa vyama hivyo wanatakiwa kuwa na utashi wa kisiasa kwa kujenga umoja
miongoni mwao na kujenga utamaduni wa kutumia ushawishi badala ya vurugu
Msajili huyo amesema vyama vya upinzani vinatakiwa
kuikosoa serikali kwa misingi ya sheria ili iweze kutekeleza mipango ya
maendeleo kwa wananchi ambao wamekuwa wakilalamika kila uchao kuhusiana na
masuala mbalimbali.
katika hatua
nyingine Bwana Tendwa amesema kuwa
sheria ya uchaguzi inatakiwa kufanyiwa marekebisho ili kuruhusu vyama vya SIASA
kuungana katika kugombea nafasi fulani kama urais au ubunge kwa ajili ya ustawi
wa demokrasia hapa nchini.
Kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi,Msajili amesema ni
sheria muhimu kwa ajili ya maadili ya viongozi na pia kupunguza vitendo vya
rushwa kwani viongozi wakipatikana kwa njia ya Rushwa wanaweza kuingia katika
vitendo vya kifisadi ili kurejesha fedha walizotumia nyakati za uchaguzi.
Msajili huyo amezitaka taasisi za kisiasa kuwa huru katika
kutoa maoni ya katiba kwani kila mwananchi na jumuiya mbalimbali zina uhuru wa
kuchangia kwa mujibu wa sheria na haki za binadamu.
Tanzania imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwa Mfumo wa
siasa wa vyama vingi mwaka 1992 ambapo vyama vilivyoanza vilikuwa 13 lakini
vimeongezeka kufikia vyama 20 mpaka sasa.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Post a Comment